Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo USWAZI. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo USWAZI. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, 5 Agosti 2013

MABINTI WA KIZARAMO NA MAFIGA MATATU-DHANA ILIYOPOTOSHWA NA WAHUNI

Inaamini kwa watu wengi kwamba, wasichana wa Kizaramo wanapowekwa ndani, hufundishwa kwamba, wakiingia kwenye ndoa ni lazima wawe na mafiga matatu.

wanaoamini hivyo wanabainisha kuwa mafiga hayo matatu ni ishara ya wanaume watatu, yaani MUME, HAWARA MPYA na BWANA WA ZAMANI. lakini pia wapo wanaodai kwamba mafiga hayo matatu ina maana ya kuolewa mara tatu katika maisha yake. Hii ikiwa na maana kwamba, mwanamke wa kizaramo ni lazima aolewe na kuachwa mara tatu maishani mwake.