Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo JAMII. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo JAMII. Onyesha machapisho yote

Jumanne, 20 Agosti 2013

KUTANA NA MWANAMKE MWENYE RASTA NDEFU DUNIANI


Pamoja na kuonywa na madaktari kuwa urefu wa nywele zake unaweza kumsababishia tatizo la kupooza, Asha Mandela amesema hawezi kuzikata.

Mama huyo mwenye mtoto mmoja aishiye Atlanta, Georgia amesema: Nywele zangu zimekuwa sehemu yangu. Ni maisha yangu. Sitozikata kamwe. Kuzikata itakuwa ni kama kujiua. Itakuwa ni sawa na zombie.’

Mrs Mandela, 47, anashikilia Guinness World Record kwa kuwa na rasta ndefu zaidi duniani zenye urefu wa futi 55.

Humchukua siku mbili kuziosha na kuzikausha nywele zake. Mrs Mandela, ana mtoto mwenye miaka 11 aitwaye Zion aliyezaa na mume wake wa pili, anasema nywele zake zimesaidia uhusiano wake na mumewe.

Kwa sasa ameolewa na mume wa tatu na asili yake ni Trinidad and Tobago. Alianza kuzitunza nywele hizo miaka 25 iliyopita


Jumanne, 6 Agosti 2013

KUTANA NA VAILET MAMA WA WATOTO 2 ALIYEKIMBIWA NA BABA WA WATOTO WAKE KUTOKANA NA ULEMAVU

Mama Vailet Nyamanga (41) akiwa na Mtoto wake Rose Nyamanga (9) wakikatiza katikati ya mitaa ya Nkuhungu Wilaya ya Dodoma Mjini katika Mkoa wa Dodoma, hivi karibuni. Rose ni mwanafunzi wa darasa la pili katika shule msingi Nkuhugu, Mama huyu, Vailet, ambaye ni mlemavu wa viungo mwenye urefu wa futi mbili, Anaishi