MAHUSIANO

Getting enough sleep is  important, because how you sleep impacts on your health. So how do you sleep?


On your back
Sleeping on your back with your arms at your side is generally considered to be the best sleeping position for spine and neck health as long as you don’t use too many pillows. Buct sleeping on your back could make you to snore more than in any other position.
Experts say sleeping on your back may also help to prevent facial wrinkles and skin breakouts.

Stomach
Sleeping on your stomach can improve digestion but can put strain on the neck because you need to turn your face sideways in order to breathe. Sleeping face down can also cause back pain, as the curve of the spine is not supported.

Fetal position
Sleeping  like a fetus can have you sleeping like a baby if you typically have problems with snoring or if you’re pregnant. This position curled up with knees drawn up and  chin tilted down might be comfortable but is bad for the back and can restrict deep breathing.

Side
When you’re sleeping on your side with both arms down, the spine is best supported in its natural curve. This can definitely help reduce back and neck pain while also reducing sleep apnea. But this can contribute to acial wrinkles and sagging bréasts.

Any side sleeping can cause shoulder and arm pain due to restricted blood flow and pressure on the nerves, which may be worsened by having your arms out in front.

On your right side
If you’re a side-sleeper, which side you sleep on also makes a difference. Sleeping on the right side can worsen heartburn while sleeping on the left side can put strain on internal organs like the liver, lungs, and stomach. For pregnant sleepers, doctors advise sleeping on the left side, since this can improve circulation to the fetus. You can get a better night’s rest with less pain in the morning by supplementing your body with a pillow.


DID U KNOW THIS




 

MAMBO YANAYOMFANYA MTU AYACHUKIE MAPENZI 




SIJUI wewe ulikuwa una malengo gani wakati unafikiria kuwa na ambaye unaye; wapo ambao walikuwa na malengo kwamba akiwa na mwanaume, maana yake awe ndio sawa na mashine ya kutolewa fedha maarufu kama ATM.

Ikiwa ulichokuwa unatafuta ni mwanaume au mwanamke ambaye kwako atakuwa ni ATM, kwamba ndiye awe anakupa kila kitu unachotaka, ikiwa hatakuwa na fedha si rahisi mkaendelea kuwa na uhusiano mzuri, kwa kuwa mpango wako haukuwa mapenzi, bali kuchuma fedha na kula raha. 
Wajinga ni wale ambao wanaingia kwenye mapenzi ili kusaidiwa tu, badala ya kusaidiana. Mwenye hekima ni yule ambaye anafahamu kwamba kuingia kwenye mapenzi, maana yake ni kuongeza timu ya kusaidiana katika maisha, si vinginevyo.

Mwanamke yeyote ambaye anafikiri yuko na mwanaume maana yake ni kwamba awe anamnunulia kila kitu, kwamba kwake mwanaume ni kila kitu, kinywaji anunuliwe, chips anunuliwe nk...kwamba yeye ni mtu wa kupewa tu ofa, maana yake ni kwamba akili yake imekufa.
 

Kufikiri kwamba kuoana na fulani maana yake ni sasa yeye atakuwa anakusaidia kila kitu milele na kwamba asipofanya hivyo utamdharau, si kitu sahihi.
 

USIWE NA MATARAJIO MAKUBWA UNAPOINGIA KWENYE NDOA
Unapoingia kwenye ndoa, usiwe na matarajio makubwa sana mazuri. Jambo unalopaswa kufahamu ni kuwa uhusiano ni suala la kawaida, kwamba unakuwa na mtu kwa lengo la kuwa nae kama timu moja kusaidiana katika kuleta maendeleo.

Kati ya mambo yanayofanya watu kutofurahia mapenzi, ni pale anapotishwa kwamba labda asipofanya hiki kwa mfano kukusaidia, basi uhusiano wenu utaharibika.
 

Kuna wanawake utasikia aaah sasa kuna maana gani ya kuwa na mwanaume ikiwa namwomba fedha hawezi kunisaidia? Fikra kama hii ni ya kipuuzi. Wewe kwanini huna fedha? Ndoa ni kusaidiana, sio kugeuzana ATM.
 

YUKO BIZE NA SIMU, KOMPYUTA NK
Kati ya mambo yenye kutiana ‘kichefuchefu’ katika mapenzi ni pale kwamba uko na mwenzi wako, lakini ni kama wewe ni tambala la deki; yaani yuko bize na simu yake au kompyuta au kitu kingine chochote.

Wengine unakuta labda anawasiliana na wengine kwa mitandao ya kijamii kama vile facebook, twitter nk, kumaanisha kwamba wewe ni muhimu, walio muhimu ni wale ambao anawasiliana nao huko.
 



KUKOSOANA MBELE ZA WATU AU HATA KUPIGANA
Wapo watu wamekuwa na tabia ya kukosoana au hata kupigana mbele za watu. Kati ya makosa yenye kukera na huenda ukasababisha uhusiano ukabaki historia ni hii...ni vizuri ndugu yangu kujifunza namna ya kuachana na hasira kali.

MATUMIZI MABAYA YA FEDHA NA KUTOKUWA NA MIKAKATI KATIKA MAISHA
 
Kila mtu Duniani anataka maisha bora, kwa maana hiyo ni furaha ya kila mtu kuona mwenzi wake anakuwa mwenye mikakati imara katika kuimarisha maisha yao.


Tabia kama za ufujaji wa fedha, kutokuwa na mikakati katika maisha, ni kati ya mambo yanayochangia ndoa au uhusiano wa mapenzi kuwa mbaya.

HUDUMA KWA WATOTO NA FAMILIA

Ukiwa kama baba au mama, unapaswa kutafakari vizuri nafasi yako katika malezi ya familia. Ni furaha ya mke na mume, kuona mwenzi wake anajali watoto na familia kwa ujumla. Je, wewe ukoje? Pata muda kufakari hali ya maisha yako, chukua hatua. 

UCHAFU NA KUTOWAJIBIKA 


Kuna watu wamekuwa wachafu kupindukia, hata kuoga kabla ya kulala ni shida, wengine kuvaa nguo mpya ya ndani hadi awe na ahadi ya kuonana na nesi au daktari. 

Lakini zaidi ya yote, ni muhimu wanaume na wanawake wakafahamu kila upande kwa kawaida huwa na nafasi yake ya kuwajibika. 


Hata kama wote mna ajira au fedha, mume anapaswa kuangalia namna ya kumfanyia mkewe mambo kama kununua nguo, chakula ndani nk...kuna wanaume hawa hawajui wake zao wamevaa nini wala hawajui ndani chakula kinanunuliwaje...hili ni kosa. Ndoa ni kusaidiana, kila upande uwajibike, ni nzuri kuwa na vikao vya namna ya kuendesha ndoa yenu.

 

 

Fahamu namna ya kuishi na mpenzi anayependa fedha!

 
HAPA tunazungumza kuhusu mapenzi kama kawaida yetu. Leo nimekuja na mada ambayo naamini itawagusa wengi. Marafiki zangu, kusaidia katika mapenzi ni jambo zuri tena lenye mantiki sana.
Suala la kusaidiana si la upande mmoja. Linaweza kuwa kwa wote, kwa mwanaume au mwanamke. Ni kati ya nguzo muhimu katika mapenzi, lakini kwa bahati mbaya kuna wale ambao wamekuwa na tabia ya kupenda sana fedha!
Unajua wenzi wanajuana kulingana na wanavyoishi, hivyo ni rahisi sana kumgundua mwenzako kama anapenda sana fedha au ni kweli ana tatizo linalohitaji msaada wako. Hii ni kasoro, lakini haimaanishi kwamba ndiyo sababu ya kuachana.
Katika mada hii ipo dawa ya namna ya kudumu katika mapenzi motomoto na mwenzi wa aina hii. Imekuwa ni kawaida kumsikia msichana akitamba mbele ya wasichana wenzake kwa kusema: “Mimi nina kibuzi changu bwana kila ninachotaka kinanipa, kinajua kisiponipa nakitosa tu, yaani nakichuna kama sina akili nzuri.”
Umewahi kukutana na maneno ya aina hii? Bila shaka jibu ni ndiyo. Si hivyo tu, wapo wanaume pia ambao ni kero kwa wapenzi wao, yaani wamegeuka wanaume kama mabinti kwa tabia zao za kutegemea kupewa kila kitu na wapenzi wao hata kama wanao uwezo wa kuvipata vitu hivyo kama watajishughulisha.
Ninachotaka kusema leo ni kwamba, mapenzi ya kweli hayana uhusiano wowote na fedha, ukiona mpenzi wako anaweka fedha mbele na ukishindwa kumpatilizia anachokitaka anakasirika, jua penzi lake lina walakini, hakupendi bali anataka kukutumia kisha kukuacha.
Katika mapenzi hatukatai suala la kusaidiana, mpenzi wako akiwa na shida fulani akaomba umsaidie, kama unao uwezo msaidie na kama huna mueleze ukweli kisha muangalie namna nyingine ya kumsaidia.
Itakuwa siyo busara kama utakuwa na tatizo lakini ukaona kwamba ukimweleza mpenzi wako ataona unamchuna. Wapenzi wanaopendana kwa dhati hawachunani bali wanasaidiana na hili ni kwa pande zote mbili.
Kinachokera ni kutoishiwa na matatizo na wakati mwingine unakuta kuchuna kwingine ni kwa mambo ya starehe. Yaani sasa hivi umemuomba mpenzi wako vocha, hajakaa vizuri umemtaka akija akuletee chipsi mayai, baadaye unataka akutoe ‘out’, bila kujali kwamba wakati huo mpenzi wako ana fedha au laah.
Katika mazingira hayo unadhani mpenzi wako atashindwa kukuchoka? Akikuacha kwa sababu hiyo utamlaumu? Kimsingi ukiwa na mpenzi mwenye tabia ya kutaka kukuomba fedha kila wakati tena katika matumizi mengine ambayo siyo ya msingi, mbinu zifuatazo ni muhimu kuzifuata. Twende tukaone.
MWELEZE UKWELI
Kama huna fedha wakati mpenzi wako anakuomba, mueleze wazi kuwa huna na kamwe usijaribu kutoa ahadi ambazo huenda ukashindwa kuzitimiza. Usiwe mtu wa kutoa ahadi za uongo, mara nitakununulia hiki na kile.
Mwanaume hatakiwi afahamike siku ana fedha au hana. Maana kuna wenzangu ambao siku za mishahara wanabadilisha hadi kutembea! Mwanamke akijua hilo naye ataongeza ‘mizinga’ ili afaidi.
JENGENI KUSAIDIANA
Jambo la muhimu ambalo wanaume wengi wanalisahau ni kutokuwafundisha wapenzi wao wajibu wa kutoa. Utakuta kila kitu ananunua yeye, hata nauli ya basi analipa, wakati mpenzi wake ana kazi yake.
Ifike wakati kwa makusudi, mwanaume ampe majukumu ya kufanya mpenzi wake, hiyo itamsaidia mwanamke kujua namna fedha zinavyokuwa hazitoshi na ataweza kubana matumizi.
ACHA UFUJALI
Kuna wanaume wengine tangu wanatongoza wanakuwa ni wafujaji wakubwa wa fedha kwa kutoa ofa na zawadi kibao. Hii inaweza kumjengea imani mpenzi wako kuwa unazo!
Unachotakiwa ni kudhibiti mapema matumizi yako hata kama fedha itakuwepo. Ifahamike kuwa kutoa hakushibishi uhitaji, kadiri unavyotoa ndivyo unavyoongeza mahitaji. Weka maisha yako katikati usijidai tajiri kumbe ni kapuku tu.
BAKI NA HILI
Katika kumalizia niseme tu kwamba, mapenzi si kukomoana, bali kusaidiana. Jenga tabia ya kumsaidia mwenzako ili siku na wewe ukiwa na tatizo akusaidie.
Kitu unachotakiwa kukiepuka ni kuwa tegemezi hadi unakuwa kero. Kumbuka kumpiga mizinga mpenzi wako kila mara kunapunguza mapenzi hivyo epukana na tabia hiyo.

 

Hasara 5 za ushauri wa rafiki kimapenzi.


Watu wengi wamekuwa wepesi kukimbilia kwa rafiki zao ili kuomba msaada wa mawazo ya nini wafanye kwenye mapenzi. Imani iliyojengeka kwa watu wengi katika jamii yetu ni kuwa, ushauri ni kitu muhimu sana kwa kila hatua.

Kwa mtazamo wa haraka haraka unaweza kuishia kwenye ukomo huo wa fikra na kuamini juu ya ushauri wa mtu kukufikisha mahali sahihi kwenye mapenzi. Unapokerwa na mpenzi wako unakimbilia kushauriwa na wakati mwingine hata unapotaka kuoa au kuachana na umpendaye, unamuomba rafiki yako ushauri.

Je, umeshawahi kufikiria hasara za kuomba ushauri wa kimapenzi kwa rafiki yako? Hebu ungana nami wiki hii ili nikumegee kidogo hasara za ushauri.

UTAKUPOTOSHA
Ni wazi kwamba kipimo cha uelewa kinatofautiana kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine. Ifahamike kuwa, uhodari wa mambo nao hutofautiana, mtu anaweza kuwa mahiri katika siasa na akaaminika kwenye jamii, lakini ukimpelekea suala la mapenzi anakuwa hajui kitu, hivyo ni rahisi kukupotosha.

Uchunguzi unaonesha kuwa, wapenzi wengi hupotoshwa na rafiki zao wasiokuwa na uelewa wa kutosha juu ya tatizo au suala husika la kimapenzi. Ni vyema kuwa makini unaposhauriwa.

UTARAHISISHA MAMBO
Mara nyingi washauri huwa si wao wanaokabiliana na mambo, hivyo ni rahisi kwao kupima vitu kwa juu juu tu na kushauri kirahisi rahisi.
“Vipi kakupiga namna hii, aaa huyu si mwanaume kwa kweli ni bora ukaachana naye.” Anasema ni bora kuachana naye kwa sababu haumizwi na kuachana, unayeachana ni wewe anayekushauri.

“Mkubali tu bwana unalaza damu, hiyo tabia yake ya uhuni atabadilika, shosti unataka kuacha bahati ipite?” Kwa mshauri ni rahisi kusema hivyo lakini kumbuka ukubwa wa tatizo hatimaye utakabiliana nao wewe. Hii ina maana kwamba, unapofikiria kuhusu ushauri ufikirie pia kuhusu kushauriwa jambo kirahisi, ukiuvaa mkenge mwenye kuumia utakuwa ni wewe.

UTAKUGEUZA
Ulimwenguni kuna aina zaidi ya 1000 za mapenzi na kila mmoja anatajwa kupenda kwa staili yake. Mapenzi ni kama chembe hai nyekundu zilizopo kwenye damu ya mwanadamu ambazo zinaelezwa na wataalamu kuwa hazifanani hata kidogo. Uzoefu unaonesha kuwa, washauri wengi hushauri kwa uzoefu wao, lakini je, ni sahihi uzoefu huo uwe msaada kwa mtu mwingine?

Jibu ni hapana, kinachotokea mara nyingi kwenye ushauri ni mtu kumfanya mwenzake awe kama yeye alivyo, yaani apuuze, aamue na apende kama staili yake, jambo ambalo haliwezekani kabisa kwenye mapenzi. Vipi Juma ageuke ghafla awe kama Hassan kwenye suala la mapenzi? Ushauri ni muhimu lakini upime kama unalingana na matakwa yako.

UTAKUONDOLEA UJASIRI
“Kwa maelezo hayo mumeo ni malaya sana, naona itakuwa vigumu kumbadilisha, ni bora ukaanza maisha yako kwa sababu kuna siku hali itakuwa mbaya.”
Huu ni ushauri ambao unaweza kumuondolea mtu ujasiri wa kukabiliana na tabia ya mumewe hadi kufikia hatua ya kumsaidia akaachana na tabia zake mbaya.

Ushauri huondoa ujasiri wa kukabili tatizo hasa pale anayekushauri atakapolipeleka suala lako kwenye njia ngumu isiyokuwa na ufumbuzi. Ikumbukwe kuwa, anayeamini kushindwa ni mshauri lakini wewe kama mwanamke unaweza kusimama kutetea penzi lako na kuliweka sawa mpaka jamii ikasema: “Jamani huyu dada kamrekebisha kweli mumewe, hakuwa hivi alikuwa mlevi lakini sasa kaacha pombe.

UTAKUNYIMA FURSA
Kwenye mapenzi kuna fursa nyingi za mafanikio ambazo unaweza usizipate ukiwa mtu wa kusikiliza sana ushauri wa watu. Kuna wakati ambao unatakiwa usimame wewe kuamua kumpenda mtu ambaye jamii inaona kama utapotea.

 

Ukitaka salama kwenye mapenzi, usifanye makosa haya

 
TUNAPENDA kuongozwa na fikra zetu. Kila mmoja anataka mwongozo wa maisha yake uendane na halmashauri ya ubongo wake. Hufanya hivyo, bila kujua kuwa kuna kikomo fulani ndani yake. Akili na matakwa ya moyo, wakati mwingine vinaweza kukupoteza.
Moyo unaweza kumpenda mchawi na ukawa huelewi kitu kwa chochote utakachoambiwa. Penzi la jambazi likikuingia, serikali ndiyo utaiona ni katili kwa sababu inamsaka mwenzi wako usiku na mchana. Hii ina maana kuwa mapenzi ni zaidi ya fikra za kila mtu.
Hutokea watu kuachana wakati bado wanapendana. Migogoro midogo inawafanya watengane, matokeo yake kila mmoja anabaki akiumia kivyake. Huo ni mfano mmoja kati ya mingi inayoonesha kwamba mapenzi yapo juu ya fikra za kawaida. Inahitaji utulivu wenye mashiko ya sayansi ya saikolojia.
Kuna ambao waliishi kwa mategemeo ya kuachana. Wakiamini wamechokana, matokeo yake kwenye ubongo wao wakatengeneza maneno: “Ipo siku.” Hata hivyo, miezi na miaka ikakatika mpaka wakazikana. Kumbe Mungu aliwaandikia wawe pamoja mpaka kifo ila wao hawakujua.
Dosari ya aina hiyo inatokana na wawili wanaopendana lakini upendo wao ukapofushwa na migogoro ya hapa na pale. Nasisitiza kuwa watu ni lazima wagundue mapema matatizo yao kabla ya kuhisi kwamba kati yao hakuna mapenzi. Vilevile, kila mmoja amuelewe mwenzi wake ni binadamu na siyo malaika.
Ana mapenzi naye, tena mapenzi makubwa. Hata hivyo, hiyo haimfanyi awe malaika. Ni binadamu, kwa hiyo wakati anadumisha mapenzi yake, anaweza kufanya makosa mengi. Jaribu kumvumilia kwa sababu ameumbwa na udhaifu, hajakamilika.
Baada ya utangulizi huo, ni vizuri kujua kuwa yapo makosa ambayo wengi huyafanya, tena mara nyingi bila kujua. Tunaishi nayo, matokeo yanakuwa ni mazoea. Hata hivyo, mara nyingi hutokea yanaharibu uhusiano ndiyo maana nimechagua tuyajadili. Yafuatayo ndiyo makosa yenyewe:

KULICHEZEA KAMARI PENZI LAKO NA MAISHA YAKO
Hapo ulipo hujawahi kuona mtu anapambana kuhakikisha mwenzi wake anabadilika tabia? Bila shaka tayari ulishajionea. Je, umejifunza nini kutoka kwao? Ni kweli kabisa kwamba mwenzi wako si malaika, kwa hiyo mnapokutana lazima mtatofautiana, je, ikitokea hamuendani kabisa?
Umejitahidi kumuweka kwenye mstari unaotaka lakini mwenzako haendi. Unasubiri nini? Kung’ang’ania penzi la mtu ambaye huendani naye, ni sawa na kuuchezea kamari moyo wako, vilevile ni sawa na kuyachezea karata tatu maisha yako.
Upo na mwenzi wako ambaye hakutoshelezi. Mnakutana mara nyingi lakini hakufikishi pale unapotaka upelekwe na mwandani wako. Unanyamaza tu kwa imani kuwa ipo siku ataweza, siku zinakwenda na mabadiliko hayaonekani. Unajipa matumaini kedekede kwamba kuna siku nyoka ataota miguu na jongoo atakuwa na macho.
Unakuwa na mpenzi ambaye kila siku anakupa visingizio ili msikutane faragha. Je, kwa nini usijiongeze kwamba mtu huyo hana hisia na wewe? Au, kwa nini usijiulize kama pengine mtu wako yupo kwenye uhusiano wa pembeni ambako anatoshelezewa mahitaji yake?
Tatizo kubwa ambalo inatakiwa lijulikane ni kwamba wengi wanapoingia kwenye uhusiano, hawapimi watu wao ni wazuri kwao kiasi gani. Wanavutwa na matamanio ya juu. Mvuto wa juu, huipumbaza akili na kudhani moyo unapenda kumbe ni uongo mtupu.
Mtu anaweza kudumu na mwenzi wake ambaye hamtoshelezi kwa miaka mingi. Anapumbazwa na mvuto wa juu, kwa hiyo anashindwa kuelewa mantiki ya muungano wa nyoyo. Zingatia kwamba mwenzi wako ambaye nyoyo zenu zimeungana, lazima atakuridhisha, naye ataridhika kwa huduma unayompa.
MFANO: Jayden Brown anatoa ushuhuda: “Nikifikiria uhusiano wangu uliopita nabaki najishangaa. Nilikuwa mbinafsi, nilikuwa naoneshwa upendo na wapenzi wangu lakini nilikuwa sitoi ukilinganisha na wao. Nilishangazwa na wanawake waliojitoa kwangu, wao waliamini kuna siku ningebadilika.
“Wanawake niliokuwa nao, walijipa matumaini kuwa ni muda tu, kipo kipindi ambacho kingefika na maisha yetu yangekuwa salama. Kumbe walichowaza wao, hakikuwa ndani ya akili yangu.
“Wao waliamini kwamba upo muda wa mabadiliko ya mimi kuwa mtu bora, ningebadilika kuwa mwema kwenye mapenzi, ningekuwa mpenzi bora. Kitu mapenzi juu yao hakikuwa ndani yangu kabisa.”

 

NAMNA YA KUBADILI MAUMIVU YA MAPENZI KUWA FURAHA

 
BILA shaka mpenzi msomaji umzima buheri wa afya na muda huu unanifuatilia katika busati letu zuri la mahaba, mahali tunapojuzana na kuelimishana mambo kadha wa kadha yahusuyo mapenzi na uhusiano. Nakukaribisha kwa moyo mkunjufu tuijadili mada yetu ya leo kama inavyojieleza hapo juu.
Ni ukweli usiopingika kuwa katika zama hizi za sayansi na teknolojia, maumivu ya mapenzi yameongezeka maradufu. Kile tunachoamini kuwa ni maendeleo, kinazidi kuzitesa hisia na nafsi zetu na suala la kutendwa, kuumizwa, kuvunjika mioyo au kusalitiwa, linaonekana kuwa fasheni siku hizi.
Kinachowasumbua wengi ni kushindwa kuelewa nini cha kufanya baada ya kuangukia katika dimbwi la maumivu ya kimapenzi. Hebu kila mtu ajiulize:
Umewahi kukuta SMS ya mapenzi kwenye simu ya mpenzi wako akimtumia mtu mwingine tofauti na wewe? Ulijisikiaje uliposikia mtu mwingine akiitwa majina mazuri ya kimapenzi  na mpenzi wako, pengine kuliko hata yale ambayo huyatumia kwako? Ulichukua uamuzi gani?
Kila mtu ataeleza anavyojua yeye lakini ukweli ni kwamba wengi hawajui kukabiliana na maumivu hata yale yanayosababishwa na maisha ya kawaida. Kwa kuwa maumivu, usaliti, kuvunjika kwa mioyo na uongo katika mapenzi ni jambo ambalo kwa kiasi kikubwa halikwepeki katika zama hizi, jambo la msingi ni kujua nini cha kufanya baada ya kutokewa na dhoruba hizo za kimapenzi.
Hebu msikilize msomaji wangu, Jane wa Ilala Bungoni jijini Dar, alivyokuwa analalama:
“Wiki nzima inaisha sasa, siendi kazini, chakula hakipandi, usingizi sipati wala sitamani kitu chochote, kitu pekee ninachokifanya ni kulia usiku na mchana, naomboleza na kulalama katika kila sekunde inayopotea mpaka natamani kujiua, sioni tena thamani ya kuishi, nayachukia mapenzi, nawachukia wanaume,” alisema Jane huku akilia kutokana na kutendwa na mwandani wake aliyemsaliti kwa kutoka na rafiki yake kipenzi.
Yawezekana Jane hayuko peke yake, wapo wengi ambao wanateswa sana na mapenzi lakini hawana sehemu ya kuyatoa maumivu yao, wanaumia ndani kwa ndani, miili yao inadhoofika kila siku, hawana furaha japokuwa wanapata mahitaji yote muhimu, chanzo kikuu kikiwa ni mapenzi.
Hapo ndipo ninapoona umuhimu wa kila mmoja kujua namna ya kusimama tena pale anapoangushwa na maumivu ya kimapenzi.
Zifuatazo ni mbinu ambazo zitakusaidia kuyabadilisha maumivu yako ya kimapenzi kuwa furaha.

JIFUNZE KUSAMEHE NA KUSAHAU
Hakuna jambo ambalo hutuliza fikra na hisia za mapenzi kama kukubali kumsamehe yule aliyekuudhi kabla hata hajakuomba msamaha na kuamua kusahau yote yaliyotokea. Yawezekana wengi mtasema haiwezekani. Inawezekana na wote waliojaribu mbinu hii walifanikiwa.
Marafiki, lazima kila mmoja aelewe kwamba unapokasirika au kuumizwa, anayeteseka siyo yule aliyekusababishia maumivu bali ni wewe mwenyewe. Hasira au maumivu ya kimapenzi huwa kama moto mkali ambao huitafuna taratibu nafsi ya mhusika.
Ukisamehe maana yake unaupa moyo na akili yako nafasi ya kupata sehemu ya kutulia na kuuzima moto ambao tayari ulishaanza kukolea ndani yako.

 

FAHAMU MAMBO YANAYOWEZA KUSABABISHA UPENDO UKAPUNGUA KWA MPENZI WAKO

1. UGOMVI WA KILA SIKU
Kwenye Ulimwengu Wa Mapenzi Hakuna Kitu Kibaya Kama Kutoweka Kwa Amani Kaa Ukijua Mapenzi Ni Matamu Na Yanaraha Iliyoambatana Na Furaha Hakuna Mtu Anaependa Kuishi Bila Ya Kuwa Na Furaha Hivyo Ikitokea Katika Mahusiano Wapenzi Hawapatani Na Kila Mmoja Wao Hataki Kukubali Kosa Wote Wanajiona Wapo Sahihi Halafu Mwisho Wa Siku Wanapatana Ghafla Bila Kuombana Msamaha Ni Wazi Kabisa Kosa Bado Litakuwa Halijarekebishwa Hivyo Ni Rahisi Kutokea Tena Ugomvi Na Ikitokea Kila Siku Penzi Lenu Linatawaliwa Na Ugomvi Nirahisi Penzi Kukosa Muelekeo Na Kila Mmoja Wenu Akahisi Hapati Amani Ya Pumziko La Moyo Kwa Mpenzi Wake Hivyo Mnaweza Kujikuta Upendo Unapungua Katika Penzi Lenu Na Matokeo Yake Moyo Wako Utakuwa Bado Haujapata Kimvuli Cha Burudani Za Mahaba Utajiwa Na Fikra Za Kutaka Kumtafuta Mpenzi Mwingine.

2. KUTOKUBALI HALI HALISI YA MPENZI WAKO:
Hii Ni Moja Kati Ya Sababu Kubwa Inayopunguza Mapenzi Kwa Kiasi Kikubwa, Walio Wengi Katika Mahusiano Siku Zote Hutegemea Faida Tu Kwa Upande Wake Pasipo Kumjali Mwenzake Zaidi Hili Hutawala Katika Upande Wa Kifedha, Unaweza Kumkuta Mtu Anampenda Mpenzi Wake Pindi Awapo Na Hela Na Kama Ikitokea Siku Mpenzi Wake Kakosa Hela Basi Inaweza Kutokea Hali Ambayo Si Yakawaida. Kikubwa Naomba Utambue Kuwa Mapenzi Sio Pesa Ila Pesa Ni Sehemu Moja Wapo Ya Mapenzi Ambayo Hutumika Katika Njia Ya Kuboresha Mapenzi Nachoweza Kukwambia Jaribu Kuwa Muelewa, Kubaliana Na Hali Halisi Ikitokea Unashida Ya Pesa Au Kitu Chochote Toka Kwa Mpenzi Wako Muombe Kama Anacho Atakupa Au Kukununulia Na Kama Hana Atakuambia Kwamfano: "Mpenzi Kwa Sasa Hali Yangu Iko Chini Kidogo Naomba Univumilie Kati Ya Hizi Siku 2 Nitakupa" Utakapo Ambiwa Hivi Kuwa Nasubira Mvumilie Ila Kama Hutojali Hali Ile Na Ukaenda Kinyume Na Maombi Yake Niwazi Kabisa Hisia Zake Zitamtuma Wewe Si Mkweli Kwake Na Nirahisi Kupunguza Upendo Kwako

3. KWENDA KINYUME NA HISIA / MATAKWA YA MPENZI WAKO:
Mpendwa Napenda Ufahamu Katika Mapenzi Kila Mmoja Huwa Na Tabia Yake Na Sheria Zake Katika Mapenzi Hivyo Ni Vizuri Mkiwa Kama Wapenzi Katika Mahusiano Yenu Muweze Kusomana Tabia Na Kila Mmoja Wenu Aweze Kutambua Mpenzi Wake Anapenda Nini Na Nini Hapendi Tukija Katika Upande Wa Sheria Pia Ni Vizuri Kama Kila Mmoja Wenu Aweze Kumueleza Mwinzie Vitu Anavyotaka Vifuatwe Katika Mahusiano. Mapenzi Yanaweza Kupungua Katika Hili Iwapo Kama Itatokea Kuna Mmoja Wapo Kati Yenu Anahitaji Afanyiwe Vitu Fulani Lakini Vinakuwa Havitekelezwi Kwa Mfano: Mpenzi Wako Anaweza Akakuomba Kushiriki Tendo La Ndoa Akiwa Na Hamu Anakwambia "Dear Leo Naham Nawewe Mpenzi Nahitaji Kulifurahia Penzi Lako Usiku Wa Leo" Unamjibu "Umeisha Anza Nawewe Mimi Sijisikii Bwana!". Kinapotokea Kitu Kama Hiki Ni Dhahiri Kwamba Umeshindwa Kumtimizia Mpenzi Wako Mahitaji Yake Ndipo Upendo Wake Kwako Utaanza Kupungua Hatima Yake Ataamua Kutafuta Mtu Mwingine Kwani Atahisi Kama Kwako Hapati Anavyovitaka.

 

Je unasumbuliwa na tatizo la kutodumu na mpenzi mmoja?

 
Ni matumaini yangu marafiki mtakuwa mko poa na mnaendelea na majukumu ya kazi za kila siku. Kama kawaida kupitia safu hii tunapata kujifunza yahusuyo mapenzi.
Ninapoandika makala haya, najaribu kujenga picha kwa vijana wangu wakali kunako anga la muziki wa Bongo Fleva, Ali Kiba na Judith Wambura ‘Jide’ walipoimba; hakunaga mapenzi yale… kupendana ni zama za kale!... siku hizi kwa kudanganyana, mvulana msichana, ishakuwa poapoa tu.
Kizazi cha zamani hakikupata shida sana katika hili. Kilisubiri muda muafaka ufike ndipo mtu athubutu kufanya maamuzi ya kuingia katika uhusiano ambapo ndani ya muda mfupi basi ndoa ilichukuwa nafasi.
Kizazi cha sasa hivi, kimetawaliwa na tamaa, vijana wanaingia katika uhusiano wakipelekwa na tamaa za kimwili pasipo kutazama umri na madhara ya kukurupukia mapenzi. Matokeo yake sasa, ndiyo pale unapoona vijana wanateseka katika kumpata mke au mume wa maisha.
Ukweli ni kwamba, tatizo na kutodumu na mpenzi mmoja kwa sasa ni sugu haswa kutokana na mapenzi kuzidiwa nguvu na fedha au hulka ya mmoja wenu.
Ilivyo sasa, ni rahisi sana mtu kuachana na mpenzi huyu kuhamia kwa yule akitegemea kupata kitu fulani ambacho amekuwa akikikosa kutoka kwa mpenzi wake.
Ni vema sasa, tukajiuliza nini faida ya huko kuhamahama kwa kila kukicha? Matokeo yake ni nini? Hapo ndipo utagundua kwamba yule unayemfuata ukidhani atakupa suluhu ya tatizo ulilokuwa nalo kwa mpenzi wako wa awali tayari na yeye ameshatendwa sana, moyo wake hauwezi kuwa kwako moja kwa moja.
Cha msingi hapa ni kufahamu alama za nyakati na kuweza kupambanua mambo ili kuendana na mazingira uliyonayo. Vipengele vifuatavyo vitakusaidia kutambua nini cha kufanya katika ulimwengu huu ambao mapenzi yanaanza kupoteza thamani yake ili kuweza kufikia malengo.
1. TAZAMANENI VIGEZO
Kumtazama mpenzi wako inamaana kubwa sana katika uhusiano, haswa kwenye hatua za mwanzoni kabla hujafanya maamuzi kuwa mke au mume. Inakupasa rafiki kutazama aina ya mwanaume au mwanamke utakayemtaka atakuwa sahihi kudumu katika uhusiano kwa muda gani?
Jiwekee malengo ya karibu kwa kutazama utayari wa mwenzako. Tumia akili yako ya kuzaliwa kuweza kupambanua mambo ambayo hayahitaji elimu ya chuo kikuu.
Kabla ya kuanzisha uhusiano mpya tayari utakawa umeshaona mengi siku zilizopita kitu ambacho kitakusaidia kumpima mwenzi wako kama yupo tayari kuanzisha safari mpya ya mapenzi yenye malengo.
2. USIHARAKIE PENZI
Marafiki wengi kwa sasa wanapoingia katika uhusiano huwa wanafuata tendo la ndoa tu. Ni bora ukasubiri kwa muda fulani ili uweze kumfahamu mwenziyo anamsimamo gani kabla hujazama ndani ya penzi.
Tendo la ndoa ni kitu cha mwisho katika mapenzi. Kabla hujafikia kufanya tendo hilo ni vema ukawa tayari umeshapita hatua kadhaa zitakazoweza kukusaidia mwenendo wa tabia za mwenzi wako kabla safari yenu haijaota mizizi.
3. MUWEKE KARIBU
Ukaribu katika uhusiano unasaidia sana, hapo itakusaidia kutambua vitu gani mwenzio anafurahi kuvipata kutoka kwako na vipi havipendi. Yawezekana kabisa ukampatia au kumfanyia kitu anachotaka ili iweze kukusaidia mbinu nyingine za kumfanya awe karibu na wewe utamfahamu zaidi.
Ukaribu huo, utasaidia kumfahamu mpenzi wako kwa vitendo, utampima kama moyo wake ni wa kuridhika ama la! Huwezi kumfahamu mtu wakati muda mwingi unakuwa bize na mambo yako, tenga muda kila wakati uweze kuwa na mpenzi wako ili uweze kupata mambo mengi kutoka kwake.
4. JIFUNZE TABIA ZAKE
Unapojifunza tabia za mpenzi wako, ni rahisi udhaifu alionao katika uhusiano. Yawezekana ukabaini kitu ambacho ni rahisi kuweza kumbadilisha tabia zake pasipo hata yeye kujua kama unambadilisha.
Tabia ya mtu huwa haijifichi hata siku moja, hata kama ataamua kuficha makucha lakini mwisho utakuja gundua. Wengi wanaingia katika mapenzi kwa ajili ya kupata masilahi fulani huwa hawapendi kucheleweshewa hivyo atajitoa mwenyewe kabla hata moyo wako haujazama katika penzi lake.
5. ZUNGUMZENI UKWELI
Ukweli huwa ndiyo silaha kubwa katika mapenzi. Mmoja wenu akiwa muongo hakika penzi haliwezi kufika mbali. Jaribu kumwambia mpenzi wako ukweli wa hali uliyonayo huku ukitazama mapokezi yake.
Kwa mtu mwenye mapenzi ya dhati siku zote huamini katika ukweli. Epuka kuongopa, jadilini mambo yenu. Wekeni mikakati ya penzi lenu ili muweze kufikia malengo.
Ni vema ‘ukamchana live’ mpenzi wako kwa kumwambia, “najua unajua kama najua sasa kwa nini tudanganyane?” Wakati huo kila mtu ataona ipo haja ya kutulia sababu kama ni ujanja basi wote mmeshapitia nyanja zote hivyo mnapoamua kutulia basi mnatulia kweli.


 

USISTADUU, UBRAZAMENI NA MAPENZI YA KICHINA


MAPENZI yamekuwa magumu. Ni mzigo mzito kuubeba. Yanaendelea kujeruhi wengi, bado ni mateso kwa wengine. Sasa hivi, asilimia kubwa ya watu, inaamini kwamba kupata mwenzi sahihi wa maisha ni ndoto za alinacha. Ni kamari, ni bahati nasibu.
Maendeleo yamekuja na mambo leo. Kile kinachoonekana ni Uzungu, kimeathiri kwa kiasi kikubwa ustaarabu wetu. Mila na desturi zetu, vimepokwa na utandawazi uliotujia. Hii inamaanisha kwamba uhusiano wa kimapenzi wa sasa, hauendani na sura ya utamaduni wetu.
Vijijini kuna unafuu japo na kwenyewe fujo zimeshaingia na mambo yameshabadilika. Mijini ndiyo matatizo yenyewe. Ulimwengu wa digitali na fursa za mitandao zinatutia wazimu. Tunataka kuiga mitindo ya maisha ya wenzetu, matokeo yake tunageuka watumwa wa mapenzi.
Hayakuletwa mapenzi ili yawaumize watu, yapo kwa ajili ya kutoa faraja ndani ya jamii. Yalivyo ni kwamba baada ya misukosuko ya kimaisha, vurugu mechi za kusaka riziki na mihangaiko mingine ya kimaisha, angalau unaweza kusahau yote unaporejea kwa mwenzi wako.
Hata hivyo, mapenzi hugeuka matatizo pale ambapo kazini umeondoka pakiwa moto, unarudi nyumbani nako pia unakuta moto. Unakosa sehemu ya kwenda kujishikiza. Faraja inaota mbawa. Hapa ndipo tafsiri ya mapenzi inapokosa mashiko. Jitazame, muangalie na mwenzako!
Japo ni ukweli usiopingika kuwa mapenzi siku zote hayapo tambarare hata kwa wenza waliostaarabika, ila katika kundi la mabrazameni na masistaduu ni mtihani. Kuna usemi kwamba glasi hugongana kabatini, nakubaliana nao lakini kwa makundi hayo ni pasua kichwa.
Mabrazameni na masistaduu ni zao la mapenzi ya Kichina, yaani uhusiano bandia. Inawezekana akiwa kwako akajilegeza kama amefika, kumbe anao wengine wengi. Hili ni janga zito kwa maisha ya sasa. Uaminifu haupo, uzinzi na usaliti vimekuwa fasheni ya kutukuzwa.
Wengine siyo masistaduu wala mabrazameni, wapo kawaida au pengine wana muonekano wa heshima mno. Hata hivyo, ukichimbua hulka zao ndiyo utachoka. Ni wakali wa kuwapanga foleni, akitoka kwa huyu anakwenda kwa yule. Mapenzi yametawaliwa na rangi ya Shetani.
Wapo wanaobadili wapenzi kwa sababu za tamaa, lipo kundi linaloamini miili yao ni mtaji wa kupata fedha, wengine shida za maisha zikasababisha uamuzi huo wa kujidhalilisha, wapo ambao ni tabia. Bila kugusa huku na huko hatosheki. Makundi yote hayo yamezingirwa na Ibilisi.
Mume wa mtu, anapewa sifa ya ‘uchapaji’ wa vidosho. Kwamba anajua kuwapanga kila kona. Nyumba za kulala wageni, anaingia kama nyumbani kwake. Yaani wanamjua, ni mteja wao hodari. Akifika, wanampeleka kwenye chumba anachokipenda.
Wapo wanaopiga simu, yaani namba za nyumba za kulala wageni zimejaa kwenye simu yake. Akijibiwa kwamba Sinza Kumekucha hakuna vyumba, anapiga Vatican, nako akikosa anajaribu Mori. Inahitaji sala na dua kuishi na mtu wa aina hiyo. Kuna mawili, kama hatakupa maradhi, omba usijue tabia yake, atakuua kwa presha.
Mke wa mtu mkali wa mafiga matatu mpaka matano. Anaita vidumu. Anaingia hoteli na gesti bila woga. Wapo wanaodiriki kuwaingiza wanaume ndani ya nyumba zao, wakati waume zao wakiwa hawapo. Balaa likamkuta yule mwanamke wa Kenya, akagandiana na mwanaume aliyemuingiza chumbani kwake, juu ya kitanda anacholala na mumewe.
Wengine ni ujasiri wa asili, wapo wanaofanya hivyo kwa sababu wanaona fasheni. Katika kundi hili wanaorukaruka, wakijiona ni fasheni ndiyo shabaha yangu kubwa. Itapendeza zaidi mapenzi yakikaa kwenye mstari wake ulionyooka. Maana halisi isipindishwe.
Kama ambavyo Jennifer Lopez anabadili wanaume Marekani,

 

Mapenzi ni fursa, iheshimu kwa maana haiji mara mbili



 Kuna somo kubwa mno kwenye mada hii kwa sababu wengi wapo kwenye mateso makubwa ya kimapenzi kutokana na makosa yao wenyewe.
Ukisoma ujasiriamali, utaelekezwa kwamba mafanikio yako yatatokana pia na namna ulivyo na nidhamu katika fursa unazopata. Inawezekana ukawa na bahati kwenye maisha lakini utabaki kuwa si lolote endapo hutatumia nafasi zako vizuri.
Kama maisha, ndivyo yalivyo mapenzi. Hayatanyooka, wala hayatakaa vema upande wako ikiwa hutakuwa na heshima kwa fursa utakazopata. Si suala la ujana au kujipanga, muhimu kwako ni kuheshimu kile kilichopo jirani yako. Zingatia: Mapenzi ni changamoto nzito.
Ukichezea penzi lako leo kwa sababu unazozijua wewe, tambua kwamba halitakaa kwako daima. Kama yalivyo maisha kwamba yapo mfano wa kioo, ukiyachekea yanacheka, ukiyanunia nayo yananuna. Ndivyo na mapenzi yalivyo. Ukiyachezea, nayo yatakuchezea kweli.
Unapaswa kuyaheshimu. Heshima ya mapenzi ni kumtunuku mapenzi ya kweli huyo ambaye amekujia na mapenzi yake. Umethibitisha anakupenda kweli, sasa kinachokuwasha nini mpaka uunyanyase moyo wake? Fumba macho, mara nyingi bahati huwa haiji mara mbili.
Inawezekana mwenzi wako wa leo ndiye mwenye mapenzi ya kweli. Ila wewe unausimanga moyo wake kwa sababu hana fedha. Unakwenda kuabudu wenye uwezo. Fimbo ya mbali haiui nyoka, kwa hiyo unaweza kufanya lolote, naye hatakuwa na cha kufanya zaidi ya kumuachia machozi na sononeko.
Kuna watu hawajiulizi hili; huyo anayekuja kwako akitumia fedha kukuteka kwenye himaya yake, ameshatumia jeuri hiyo kwa wangapi? Endapo utaujua ukweli, utakuja kufahamu kwamba ni wengi aliwanasa kwa sababu alitanguliza fedha.
Weka akilini kwamba haji kwako kwa sababu anakupenda ila anayo jeuri kuwa hutapindua kutokana na fedha alizonazo. Sasa basi, unapomkubalia unamfanya aongeze kiburi. Kesho atatupa ndoano kwa mwingine na huo ndiyo utakuwa mwendo.
Atakutamani kwa sababu ya muonekano wako, kwa hiyo kutokana na kiburi cha fedha alichonacho, kesho akimuona mwingine atakayemtamanisha, atatumia fedha zake kumnasa. Hii ina maana kuwa mkondo wako, watapita wengi. Mwisho kabisa, utabaini kwamba uliingia katika msafara wa kenge.
Atapita kwa wenye tamaa za fedha, nawe utakuja kuingia humohumo. Hii ndiyo sababu ya kusema utajikuta umeunga msafara wa kenge. Wewe utasema unajiheshimu lakini huyo uliyeangukia kwake, hachagui.
Popote kambi, baadaye unapata jawabu kwamba umechangia mwanaume na machangudoa wengi wa mjini.
Tatizo siyo mvuto wako, wapo machangudoa wengi mjini na wanavutia kwelikweli. Kama kavutiwa na wewe na katumia ngawira kukunasa, inashindikana vipi kuvutiwa na machangudoa wengine, nao akatumia fedha kuwanasa? Tena wao si gharama, kwa maana ndiyo kazi yao.
Vilevile kwa mwanaume, atampuuza mtu anayempenda na kumvaa mwingine anayemuona anavutia zaidi. Wengi wamefanya hivyo bila kujua kwamba hao wanaovutia barabarani, asilimia kubwa ni magubegube. Unahitaji mwandani wa maisha yako, tuliza akili.
Sikukatazi kutupa ndoano, ila jaribu kufikiria mara mbili. Uliyenaye hakutoshelezi? Kumuacha mpenzi wa kweli na kujishughulisha na wengine ni sawa na mfano wa mtu aliyepoteza almasi, wakati alipokuwa ‘bize’ akitafuta mawe. Usilie kama wenzako, tuliza akili leo.
Kuna watu wanateseka leo. Wanadai wana mkosi. Eti, mapenzi yanawachapa bakora kwamba hawana bahati nayo. Kama na wewe upo kwenye kundi hili, fumba macho halafu ufikirie ulipotoka. Je, hukumuacha aliyekupenda kwa dhati? Hukuchezea moyo wa yule aliyekuwa anakujali?
Kama jibu ni ndiyo, basi hutakiwi kulia. Mapenzi yalivyo, kupata mwenye moyo mkunjufu katika kupenda ni bahati nasibu. Hivyo basi, kama ulimchezea, ni zamu yako kuteseka kwa maana uliyachezea mapenzi. Ulimpiga teke anayekupenda, sasa unahangaika na wasiokupenda. Wanakuinjoi tu.

 

Pupa katika mapenzi inapunguza uwezo wa kufikiri




Kama kawaida tunaendelea na mada zetu, nimepokea malalamiko mengi katika uhusiano, yanayotokana na mtu kupenda na kugeuzwa mtumwa wa mapenzi na kupata mateso mazito.
Kwa nini unageuka mtumwa wa mapenzi?
Wengi wamekuwa wakiteswa na mapenzi kwa vile hawakuyasoma mwanzo, matokeo yake huwa sawa na mtihani mgumu usiojua majibu yake, lazima utafeli.
Mapenzi yanasomwaje?
Wengi huyachukulia mapenzi kama starehe na kusahau kuwa ni mwanzo wa kujenga familia, tumekuwa tukiingia kwenye mapenzi kwa njia ya macho na si kutumia akili.
Nina maana gani?
Binadamu tumeumbwa na tamaa, kila kiumbe kinapenda kitu kizuri, macho huwa ya kwanza kuona na kupeleka taarifa kwenye moyo ambao nao hulipokea jambo kama lilivyo na kulitaka kwa vile ni zuri, bila kuangalia faida na hasara zake.
Hii hutokana na nini?
Siku zote pupa hupoteza uwezo wa kufikiri, hasa pale mtu anapoamini kuwa kutaka kumjua kiundani mpenzi wako ni kupoteza muda, wengi huhofia kuwa kufanya hivyo kunaweza kusababisha umpoteze mpenzi wako na akachukuliwa na mtu mwingine.
Kila mwanadamu anatanguliza tamaa ndiyo upendo unafuata, wengi wetu huwa na pupa baada ya kumtamani mtu kwa muda mrefu. Siku ukibahatika kumpata, pupa hutangulia mbele, hivyo kufurahia bahati ile na kusahau katika mapenzi kuna kitu cha ziada.
Kweli mapenzi ni bahati nasibu lakini bado tunatakiwa kupoteza muda kidogo baada ya kumpenda mtu, lazima ujue historia yake, udhaifu wake kitu ambacho kitakusaidia kurekebisha kabla ya kuingia katika uhusiano kamili.
Wengi wetu tumeponzwa na pupa, tunakuwa kama samaki, hatufikiri, baada ya kuona chambo tunameza tu bila kujua madhara yake.
Watu wa aina hii huja kushtuka wapo ndani ya uhusiano kamili, hivyo kubakia kuteseka na kugeuka watumwa wa mapenzi, kila siku kulia na kujiona una bahati mbaya kwa kulitupa penzi lako jalalani na kukosa heshima ya mapenzi.
Siku zote mwanadamu ameumbwa akiwa na sifa kuu ya kufikiri kabla ya kutenda na anayefikiri huwa hana pupa, hufikiri kwa kituo na kupata jibu kuwa hili linafaa na hili halifai.
Hata kama uliyempata alikuwa chaguo la moyo wako, kwa vile ulitanguliza pupa, sasa hivi amegeuka chukizo la moyo wako, kila siku mateso ya upande mmoja. Kabla ya kupenda jiulize unayempenda naye anakupenda?
Utamjuaje?
Uwe mkweli na muwazi, pia kuwa tayari kuishi maisha ya aina yoyote, hamuwezi kuishi maisha ya furaha mkiwa na kitu tu na kama hakuna kitu basi kero mtindo mmoja na kuiona nyumba yako kama mochwari.
Siku zote kwa muda mfupi lazima utagundua vitu vingi kwa mpenzi unayetaka kuwa naye kama udhaifu wake ambao utaufanyia kazi kabla ya uhusiano na kama hawezi kubadilika basi hakufai, bado una kazi ya kumtafuta mwingine kwa utulivu, acha pupa.

 

Fedha, uzuri si kinga ya mapenzi, kuna kitu cha ziada


WAKATI akili yangu ikianza kupata ufahamu, nilikuwa natatizika na kuwaza kitu gani hasa katika mapenzi kinaweza kumfanya mtu atulie ndani ya penzi lake. Niliamini kuwa na fedha ndiyo dawa ya mtu kumtuliza mpenzi wake au kwa mwanamke kuwa mzuri na mwenye sifa zote, ndiyo dawa ya kumfanya mpenzi wako atulie.
Baada ya kukua na kuingia katika dunia ya ufahamu wenye mitihani mingi ya mapenzi, nimegundua kuna utofauti mkubwa katika vitu nilivyoviwaza.
Wakati nakua, nilikutana na matukio ambayo niliona kama ngamia kupita kwenye tundu la sindano, lakini baada ya kupevuka, nilipata majibu ya maswali yaliyonisumbua kipindi kile cha utoto.
Sikuamini mke wa tajiri kufanya mapenzi na muuza mchicha, mwanaume mwenye mke mzuri kutembea na changudoa au msichana wa kazi asiyejua kuvaa wala kuoga.
Baada ya kuingia katika kazi hii ya kukumbushana mambo ya mapenzi, nilipata maswali mawili ya watu wawili tofauti lakini yalikuwa na jibu moja.
Mmoja alilalamika ana mke, anamhudumia kila kitu ikiwemo familia yake lakini alichomlipa ni kutembea na mtu asiye na mbele wala nyuma. Mwingine alilalamika kuhusu mpenzi wake kutembea na mwanamke wa nyumba ya pili ambaye haufikii hata mguu wake kwa uzuri.
Kabla ya kulizungumzia hilo, nirudi kwao kuwaeleza kukosa uamini hakuangalii katembea na tajiri au mwanamke anayekushinda uzuri, kutoka nje ya uhusiano au ndoa ni kosa kwa vile penzi ni la watu walioridhiana au kuoana wakiwemo waliooa wake zaidi ya mmoja.
Leo nawajibu wote kuwa fedha au uzuri wa mtu havibebi ndoa au uhusiano. Nimekuwa muumini mzuri wa kuwaeleza penzi la kweli lipo vipi, mapenzi ni upendo wa dhati kutoka moyoni, kuwa tayari kujilinda na kujiheshimu bila kujali una fedha au ni mwanamke mzuri.
Mapenzi ni mbegu inayohitaji udongo wenye rutuba ya upendo ili mbegu hiyo imee. Siku zote mwenye mapenzi ya kweli humuangalia mtu, si kitu.
Tajiri na fedha zake asipopendwa huwa katika mateso na kukonda wakati ana kila kitu. Penzi la kweli halinunuliwi kwa gharama yoyote.
Tabia ya asili huwa sawa na moto unaowaka kwenye pamba, ukitoa moshi ujue hakuna kilicho salama. Wapo watu wasiokuwa na mapenzi ya dhati, utakuta mtu anajifanya anakupenda ukiwa naye lakini mkiachana hana habari na wewe, hata kama mnakaa nyumba moja na kulala kitanda kimoja.
Mtu anapoamua kutoka nje ya ndoa wakati ndani ana mke mzuri au mume wa ukweli anayempa kila kitu, kuna mawili:
Mosi:
Huenda mwanamke aliyenaye alimtamani kutokana na sura na umbile lake na hakumpenda kwa dhati. Matokeo yake baada ya kumchoka, mwanamke huonekana hafai na hukaa naye kimazoea.
Upande wa mwanamke, naye huenda amekwenda kwa mwanaume kutokana na kujua ana fedha lakini anakuwa hana mapenzi naye. Hapo lazima atatafuta penzi la nje ili afurahishe nafsi yake, kwa hiyo watu hawa kutoka nje sishangai.
Pili:
Tabia ya kutoridhika na mpenzi mmoja, watu wa aina hii huwa hawajisikii kula kitu cha aina moja kwa muda mrefu, lazima atatafuta mtu wa kumfanya abadili mboga.
Vitu hivi vyote huwa vinawachanganya watu, hasa wale wanaoamini kuwa mwanaume anapokuwa na fedha au mwanamke anapokuwa mzuri, ni kila kitu katika mapenzi.
Mapenzi ni bahati, hasa kumpata uliyemkusudia, basi muombe Mungu utakayemchagua naye awe kweli amekukubali, hata ukiwa mbali kila mmoja amlindie mwenzake heshima, kwa kutanguliza uaminifu mbele.

 

WANAUME HUPENDA KUOA MWANAMKE WA AINA HII


WANAUME HUPENDA KUOA MWANAMKE WA AINA HII
Habari za wiki hii mpenzi msomaji. Mimi namshukuru Mungu kwa kuweza kunikutanisha na nyinyi kupitia safu hii ambayo pamoja na mambo mengine nazungumzia juu ya mada mbalimbali ambazo zinagusa maisha yetu ya kila siku.
Wiki hii nitazungumazia juu ya aina ya wanawake ambao wanaume wengi hupendelea kuoa. Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha.
Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.
Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa. Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.

 
MWEYE MAPENZI YA KWELI
Lengo kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto mara ndio wamekuwa furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake. Mwanamke asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingi utamuona macho yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.
Kwanini wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha  siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.
 
Si hivyo tu pia asilimia kubwa ya  maisha ya  ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia  ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha ya raha mustarehe.
 
WENYE TABIA NZURI
Tabia njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja suala na kuoa tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini  wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani utaambiwa  anatabia mbaya. Naweza kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya  wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.
Si hivyo tu wapo wanaume  ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.
 
WENYE UCHU NA MAENDELEO
 
Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani 'golikipa'. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini. Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.
 
WASIOPENDA MAKUU
 
Kuna  wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila wikiendi utamsikia "leo tunakwenda wapi dear?"  Akimuona rafiki yake kanunua simu ya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama  ya Grace’. Ukienda naye Pub anakuambia, "mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’. Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho  nacho na usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.

 
Wanawake kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa  kuwaoa.  Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?’ hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu fulani.’
Wanaume ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa  tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi  ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.
Kuna wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leo amemletea hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema.
Sisemi kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitaji upo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulani wakati inawezekana uwezekano haupo.
 
WAVUMILIVU
Wapo wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotea kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?
 
Uvumilivu kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.
 
Licha ya kupenda kuoa wanawake amabo wana tabia hizo nilizozitaja hapo juu, wanachukizwa sana na wanawake ambao wanavijitabia vidogo vidogo ambavyo kimsingi havikubaliki katka jamii.Tabia hizo ni kama wambea, wasio wakweli na wawazi, wasioridhika, wagumu kusamehe na wapesi wa kuchukia, wagomvi na wenye roho ya kwanini.
 Utafiti huu umefanyikwa kwa baadhi ya wanaume ambao wanatarajia kuoa wanawake ambao wanaoishi katika maeneo mbalimbali jijini Dar-es-Salaam. Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.

UKIPENDWA PENDEKA ILA USIPENDE SANA NA UWE TAYARI KUUMIZWA


MAPENZI! Hivi umeshawahi kukaa chini na kujiuliza kwamba, kama yasingekuwepo mapenzi ulimwenguni binadamu wangeishi vipi? Kimsingi ni swali gumu na hakuna anayeweza kulitolea jibu la moja kwa moja. Ni sawa na wanaume wanavyojiuliza kwamba wasingekuwepo wanawake wangeishi vipi.
Ninachotaka kukizungumzia leo ni kwamba, mapenzi yamekuwa yakiwasumbua walio wengi katika maisha yao hadi wengine kufikia hatua ya kujilaumu kwa nini wameingia katika ulingo huo.
Wapo ambao wamepoteza maisha kwa sababu ya mapenzi, wapo waliochanganyikiwa na wengine kuathirika tu kisaikolojia kwa sababu ya mapenzi. Pia wapo walioachishwa kazi kwa sababu ya mapenzi. Kimsingi mapenzi ni kitu hatari sana kama hakitawekewa umakini.
Lakini sasa licha ya mapenzi kuleta matatizo kwa binadamu, bado tunaambiwa kwamba, utakuwa peke yako kwa muda fulani wa maisha yako na mwishowe utatakiwa kutafuta mwenza ambaye utaishi naye kama mume na mke.
Swali la kujiuliza ni kwamba, je kama kila unapoingia katika mapenzi unaumizwa na mtu ambaye umempenda na ungetamani siku moja muoane, kuna ulazima wa kuendelea kung’ang’ania penzi lake? Na kama utaendelea kuling’ang’ania penzi la mtu ambaye anakuumiza kila wakati bila kujali, itakuwa inaleta maana?
Kimsingi katika maisha ya sasa hasa kwa wale ambao bado hawajaolewa au kuoa, wanatakiwa kuwa tayari kupenda na kupendwa lakini pia wanatakiwa kutopenda sana kwani madhara yake ni makubwa. Pia wawe tayari kuumizwa kwanza kabla ya kumpata yule mwenza mweye mapenzi ya dhati kwao.
Mapenzi ya sasa yamejaa usanii wa hali ya juu kiasi kwamba ukifanya uchunguzi utabaini wengi walio katika uhusiano wa kawaida yaani ‘boyfriend & girlfriend’ wanapitisha muda tu lakini uwezekano wa wao kuja kuwa kitu kimoja ni mdogo sana.
Unaweza kuwa katika uhusiano na mtu akawa anakuonesha mapenzi ya kweli mpaka mwenyewe ukajiona mwenye bahati lakini kumbe mwenzako anakufanyia usanii tu. Sasa utajuaje kwamba huyo uliyenaye hana mapenzi ya dhati kwako? Hapo ndipo penye shughuli pevu na ndiyo maana wakati mwingi tunajijengea imani tu. Tunaamini kwamba, kwa sababu ya mambo anayonifanyia mpenzi wangu, ni lazima atakuwa ameniweka moyoni mwake.
Tutambue tu kwamba mapenzi ya kujifanyisha hayawezi kuchukua muda. Utadanganya leo, utadanganya kesho lakini ipo siku mpenzi wako atabaini tu kwamba amedondoka katika penzi lisilo sahihi na hapo ndipo yaweza kuwa mwisho wa penzi hilo la bandia.
Ninachotaka kukushauri wewe msomaji wangu ni kwamba, unapotokea kuingia katika uhusiano wa kimapenzi na mtu kwa lengo la kutaka kuoana kisha yeye akaja kukuumiza kwa kukufanyia mambo mabaya, chukulia kwamba ni safari ya kuelekea kumpata mwingine mwenye mapenzi ya dhati kwako.
Najua utaumia sana lakini kutakuwa hakuna jinsi, kama yeye kaamua kukuacha huna nafasi ya kulirejesha penzi lake kwako kwa hiyo unatakiwa tu kukubaliana na hali halisi.
Ila sasa baada ya kuumizwa, hutakiwi kukurupuka kutafuta mtu mwingie wa kujaza nafasi hiyo. Hiyo ni mbaya sana kwani unaweza kujikuta unaingia tena katika penzi chungu kuliko hata lililopita. Kaa chini jiulize, mpaka kufikia mpenzi wako kukuacha ni wewe mwenye makosa au ni yeye?
Kama ni wewe lazima ujute kwanza na kuwa tayari kubadilika. Lakini kama utabaini kwamba hukuwa na kosa lolote bali uliyekuwa naye kaamua tu kukuumiza kwa sababu zake anazozijua, hilo muachie Mungu, yeye ndiye atakulipa wewe na aliyekutenda.

IWEJE ULAZIMISHE NDOA KWA MTU USIYE NA MAPENZI NAYE?


MAMBO vipi watu wangu? Natumaini kwamba mambo ni freshi na mnaendelea vyema na majukumu yenu ya kila siku. Mimi ni mzima bukheri wa afya na tunakutana tena kupitia safu hii lengo likiwa ni lile lile la kuwekana sawa katika masuala kadhaa yanayogusa maisha yetu ya kimapenzi.
Wiki iliyopita niliandika mada iliyokuwa inaeleza jinsi wapenzi wanavyoweza kujifunza kutokana na kifo cha msanii maarufu, Steven Kanumba. Ni matumaini yangu mmejifunza kitu na kubadilika itakuwa ni jambo jema kwenu.
Baada ya utangulizi huo, nigeukie sasa kwenye mada yangu ya wiki hii. Wakati flani huwa najiuliza kwa nini tunakuwa na wapenzi, kwa nini mapenzi yakawepo? Kwa nini tunaoa ama kuolewa? Kwa nini baadhi ya watu huamua kujinyonga baada ya kuachwa na wapenzi wao? Kwa nini mapenzi yamekuwa sehemu ya maisha yetu?
Kwa nini mapenzi yameharibu baadhi ya maisha ya watu? Huwa najiuliza maswali mengi na kupata majibu mengi pia.
Kwa vyovyote itakavyokuwa mapenzi ni sehemu ya maisha yetu na kwa hakika maisha yetu hayawezi kukamilika bila kuwepo mapenzi. Ninapozungumza juu ya mapenzi namaanisha yale yanayotoka moyoni mwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Mapenzi hayo hukamilika baada ya wawili hao kuwa na hisia sawa za mapenzi. Elewa kwamba kama upo katika uhusiano na mpenzi ambaye hakupendi, yaani wewe peke yako ndiyo unayempenda, wewe ni mtumwa wa mapenzi. Kama ndivyo, kwa nini ukubaliane na hali hiyo ambayo unaweza kuepukana nayo?
Unadhani hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kukupenda kwa mapenzi ya dhati na penzi hilo likawa kwa pande zote mbili tofauti na ilivyo sasa? Inawezekana! Huna sababu ya kulazimisha penzi kwa mtu ambaye unaona wazi kwamba hampendi.
Mapenzi ni nguzo ya maisha yetu, kama ukifanikiwa kumpata mpenzi ambaye atakupenda na wewe ukampenda ni wazi maisha yako yatakuwa yenye furaha isiyosimulika. Mapenzi yapo hivyo na kama ukienda kinyume chake lazima utaumia.
Wakati mwingine unaweza ukapendwa na mpenzi ambaye hujampenda, unadhani kuna ulazima wa wewe kulazimisha kumpenda? Moyo wako umeshazungumza na wewe, umekuweka wazi kuwa hauna mapenzi ya dhati kwa mtu huyo, kwa nini ujilazimishe? Tatizo hili mara nyingi huwa kwa wanawake na hao hao ndiyo wamekuwa wakiongoza kwa kutoa machozi pale wanapotendwa.
Anatokea mwanaume anampenda sana, anapomtongoza anajikuta hampendi, anachokifanya ni kumwambia kuwa atamjibu baadaye. Lengo la kumwambia hivyo ni kwa ajili ya kujipanga na kufikiria. Mapenzi hayafikiriwi kiivyo ndugu zangu.
Kama mtu unampenda, unapomuona tu siku ya kwanza, moyo wako utakuambia bila kukuficha na utabaki wewe tu kufanya maamuzi sahihi. Hii ina maana kuwa atakapokuambia anakupenda, huwezi kusubiri zaidi, hutakuwa na kitu cha kusubiri, ni nafasi uliyokuwa ukiisubiria kwa hamu sana na lazima utamkaribisha.
Tatizo lilipo
Baadhi ya wasichana wakitongozwa na mwanaume ambaye anaona wazi kuwa hampendi, lakini akawa na mali au uwezo mkubwa kifedha, huamua kumkubalia kwa lengo la kupata vitu vya mwanaume huyo.
Hufanya hivyo akijidanganya kuwa atajifunza kupenda akiwa ndani ya uhusiano na mwanaume huyo kitu ambacho hakipo katika ulimwengu wa mapenzi.
“Fedha anazo, magari anayo, hata kama simpendi nitakwenda naye hivyo hivyo mwisho wa siku penzi litajijenga lenyewe taratibu,” baadhi ya wasichana huwaza hivyo. Baada ya wazo hilo kuingia akilini mwake, huwa hana muda wa kusubiri zaidi, anakubali na wakati mwingine huweza kuingia katika ndoa.
Madhara yake
Yapo mengi, lakini kubwa ni lile la kutokutosheka na mpenzi wako uliyenaye. Anaweza akakupa kila kitu lakini ukakosa penzi la dhati ambalo ndiyo msingi wa maisha. Unajua kama kuna mtu anakupenda na wewe unampenda, unajihisi furaha na amani siku zote. Kinyume cha hivyo, furaha utakuwa ukiisikia kwenye bomba tu.
Madhara makubwa zaidi ni pale utakapojikuta ukiingia katika uhusiano na mwanaume mwingine kwa ajili ya kusaka penzi la dhati. Unajua kitakachotokea? Kama hutaleta magonjwa ndani basi siku moja utafumaniwa, lazima utafukuzwa nyumbani kwa mwanaume huyo na kama ana hasira, anaweza kukuua.
JAMBO LA MSINGI
Ushauri kwangu ni kwamba, kamwe usijaribu kuingia katika mkumbo huu wa watu wanaoingia kwenye uhusiano na watu ambao hawajawapenda.
Maisha yenyewe ni mafupi hivyo kuwa makini, fanya maamuzi sahihi yahusuyo maisha yako ya kimapenzi kwa umakini wa hali ya juu ili usije ukawa mmoja kati ya wanaolizwa na mapenzi na kuishia kujuta kila siku.

 

WEWE UNAWEZA KUWA MCHAWI WA MAPENZI YAKO


WATU wanaamini mno katika uchawi. Wanamaliza fedha kwa waganga wa kienyeji wakiamini kwamba wamerogwa, hivyo wanatafuta ufumbuzi kutoka kwa wataalamu wa mambo ya asili. Wapo wanaoita mambo ya Kiswahili.
Kwangu napinga kuita hivyo kwa sababu nami ni Mswahili na kwa uzoefu wangu, sisi Waswahili hatuna utamaduni wa kutegemea mitishamba kuamua hatma za uhusiano wetu wa kimapenzi. Ila baadhi wapo, tena wengi haswaaa!
Shika hili kwamba wewe mwenyewe pengine ndiye mchawi wa mapenzi yako. Hujiulizi kwa nini wengine wanadumu? Ni vipi wenzi wengine wanaheshimiana? Inakuaje kwako imekuwa kinyume? Siyo suala la upepo, wakati mwingine ni kujitakia.
Kivipi mwenzi wako hakuheshimu? Ni makosa gani ambayo wewe umefanya? Ukishapata majibu ya maswali hayo, utaweza kujua faida za wewe kujitambua. Nakuasa ushike moja kuu kwamba mapenzi ni nidhamu.
Yapo kama kioo, ukiyaheshimu nayo yatakuheshimu na utayaona murua. Endapo utayachukulia kwa mzaha, nayo hayatasita kukufanyia mzaha. Mwisho utakuja kugundua kwamba yanakutesa, ukifika hapo usiache kukumbuka nawe ulivyoyatesa.
Baadhi ya watu wanaamini mazoea ndiyo yanasababisha mapenzi kupungua au kuchokana. Hilo siyo kweli hata kidogo, tena nakataa kwa herufi kubwa kwa sababu wapo mabibi na mababu waliopendana tangu enzi hizo mpaka hivi sasa.
Mapenzi ni kitu tofauti sana kwenye hii dunia na hata nje ya sayari, husababisha mambo kwenda sawa au kuharibika, kuna baadhi ya vifo hutokana na mapenzi, kuna magonjwa watu nwanaumwa kisa mapenzi.
Ukipata mpenzi anayekuelewa, anakujali na anakupenda, hata dunia iwe ya tabu kwako kwa kiasi gani, utaiona inasogea kama kawaida na maisha yanaendelea vizuri tu, naamini hapo unakubaliana na mimi.
Lakini ukiumizwa kwenye mapenzi au kutopata mtu wa kukujali, kutosikilizwa basi hata kama dunia kwako ina raha, utaiona ni chungu na kama kwako dunia ni chungu tangu awali halafu ukaja kuumizwa, ndio hapo watu wanapowaza na kufikiria kujiua kwa sababu haoni hata umuhimu wa yeye kuishi.
Baadhi ya sababu zinazoweza kufanya mapenzi kupungua au mwenza wako kubadilika ni hizi;

1. KUTOSEMA KWELI
Katika mapenzi uongo ni kitu kibaya sana, uongo wa aina yoyote ile ni mbaya katika mahusiano yoyote yale na huweza kupunguza mapenzi ya dhati na uaminifu kwa kiasi kikubwa hasa kama mmojawapo atagundua kuwa mwenzi wake ni muongo, anamdanganya.
Wapo ambao wakigundua mpenzi wake ni muongo wanauliza au kuongea nao ambacho ni kitu kizuri na siku zote napenda sana kusisitiza suala la wapenzi kujadili vitu mbalimbali vinavyotokea kwenye mahusiano yao, lakini wengine wanaamua kunyamaza au kuacha kabisa.

2. KUTENGENEZA PENZI LA PEMBENI
Moja ya jibu nililolipata kwa watu wengi niliojaribu kujadiliana nao mada hii walisema kuwa, mahusiano mengine yanasababisha mapenzi kupungua, inaumiza sana kugundua yule unayempenda kwa dhati ana mpenzi/wapenzi wengine. Kubali au kataa, hii ni moja ya sababu kubwa zinazofanya mapenzi kupungua au kuvunjika kabisa.
Kamwe usimuumize moyo akupendaye kiukweli, usimfanye ajutie penzi lako,usimfanye anung’unike kwa unayomtendea, ipo siku utahitaji mapenzi ya kweli kwa mwingine na hutayapata, ukimuumiza ipo siku nawe utaumia, mapenzi ya kweli yanawezekana kama kunakuwa na uaminifu.

3. UPUUZI
Hii pia huchangia kwa kiasi kikubwa kupunguza mapenzi kama sio kuyamaliza kabisa. Unapokuwa kwenye uhusiano jitahidi kumpenda mtu wako kwa hali yoyote na usiwe na dharau kwake au hata kwa marafiki zake au ndugu zake au hata wengineo. Hakuna mtu anayependa mtu mwenye dharau hata awe nani. Hata kama mwenzi wako ana uwezo mdogo kuliko wewe, hiyo isiwe sababu ya wewe kumdharau.

4.MSEMA HOVYO
Hakuna kitu kinachoweza kumfanya mwenza wako kukukimbia au hata kukosa uaminifu na wewe kama akija kugundua wewe ni mropokaji na huna ‘kifua’ hasa kwa yale mambo ambayo ni ya chumbani na hayakutakiwa kutoka nje. Hakuna mtu anayependa siri zake kutoka hadharani na huwa inaumiza sana kwenye mapenzi kumpa mtu siri zako halafu yeye anaenda kusimulia.
Mambo mnayafanya mkiwa wawili tena ndani lakini kesho unaenda kusimulia kwa watu, si jambo la busara hata kidogo.

 

UKWELI KUHUSU KUPENDA, KUPENDWA NA KUPENDANA!


TUJADILI pamoja; Unafahamu nini kuhusu mapenzi? Najua majibu ni mengi, kuna wengine watasema mapenzi ni kupendana...mapenzi ni hisia kutoka kwa mtu kwenda kwa mwingine n.k. Kuna wakati nilishawahi kufafanua maana ya mapenzi.
Ngoja niwaambie rafiki zangu. Kwa tafsiri yangu, mapenzi ni hisia za ndani kutoka kwa mmoja kwenda kwa mwingine, hisia hizi ili ziwe sahihi ni lazima zigongane ndipo neno UPENDO huanzia hapo.
Kwa maneno mengine, wawili hawa lazima wote wawe na hisia sawa ndipo wapendane. Tunapokuja kwenye mapenzi sasa, inawapasa watu hawa wawe wa jinsia tofauti – mwanamke na mwanaume. Muunganiko wa wapenzi hawa hulenga kujenga maisha ya pamoja. Upo hapo rafiki yangu?
Yes! Mapenzi ni maisha. Kwa hakika maisha yetu hayawezi kukamilika bila kuwepo mapenzi. Ninapozungumza juu ya mapenzi namaanisha yale yanayotoka moyoni kabisa. Si maigizo.
Ikiwa upo katika uhusiano na mpenzi ambaye hakupendi, yaani wewe peke yako ndiyo unayempenda, wewe ni MTUMWA WA MAPENZI. Kama ndivyo, kwa nini uwe mtumwa?
Unadhani hakuna mwingine ambaye anaweza kukupenda kwa mapenzi ya dhati na penzi hilo likawa kwa pande zote? Inawezekana, huna sababu ya kulazimisha penzi kwa mtu ambaye hakupendi!
Mapenzi ni nguzo ya maisha yetu, kama ukifanikiwa kumpata mpenzi ambaye atakupenda na wewe ukampenda ni wazi kuwa maisha yako yatakuwa yenye furaha na hakika utafurahia maisha yako na huyo mwandani wako. Mapenzi yapo hivyo na kama ukijaribu kuyabadilisha utaumia mwenyewe!
Wakati mwingine unaweza ukapendwa na mpenzi ambaye hujampenda, unadhani kuna ulazima wa wewe kulazimisha kumpenda? Moyo wako umeshazungumza na wewe, umekuweka wazi kuwa hauna mapenzi ya dhati kwa mtu huyo, kwa nini ujilazimishe? Tatizo hili mara nyingi huwa kwa wanawake zaidi!
Anatokea mwanaume anampenda sana, anapomtongoza anajikuta kuwa hampendi, anachokifanya ni kumwambia kuwa atamjibu baadaye! Lengo la kumwambia hivyo ni kwa ajili ya kujipanga na kufikiria! Mapenzi hayafikiriwi ndugu zangu!
Kama mtu unampenda, unapomuona tu siku ya kwanza, moyo wako hutetemeka juu yake na hutamani uambiwe kitu fulani na huyo aliyeuteka moyo wako ghafla. Hii inamaana kuwa atakapokuambia kuwa anakupenda, huwezi kusubiri zaidi, hutakuwa na kitu cha kusubiri, ni nafasi uliyokuwa ukiisubiria kwa hamu sana, na lazima utamkaribisha!
‘KUJITAHIDI KUPENDA!’
Baadhi ya wasichana, akitongozwa na mwanaume ambaye anaona wazi kuwa hampendi, lakini akawa na mali au uwezo mkubwa kifedha, huamua kumkubali kwa lengo la kupata vitu vya mwanaume huyo. Hufanya hivyo ajidanganya kuwa ‘atajitahidi’ kumpenda taratibu akiwa naye ndani ya uhusiano.
“Pesa anazo, magari anayo, hata kama simpendi nitajitahidi kumpenda taratibu,” ni kauli ya kawaida sana kwa wasichana ninaowazungumzia hapa.
Baada ya wazo hili kuingia akilini, huwa hana muda wa kusubiri zaidi, anakubali na wakati mwingine huweza kuingia hata katika ndoa.
NI HATARI KUBWA!
Kuna mengi ambayo yanaweza kutokea kwa kujidanganya kuingia kwenye sehemu ambayo huna mapenzi nayo. Kubwa zaidi ni ile hali ya kutokutosheka na mwenzi uliyenaye.
Anaweza akakupa kila kitu lakini ukakosa penzi la dhati, ambalo ndio msingi wa maisha. Unajua kama kuna mtu anakupenda na wewe unampenda, unajihisi furaha na amani siku zote.
Madhara makubwa zaidi ni pale utakapojikuta ukiingia katika uhusiano na mwanaume mwingine kwa ajili ya kusaka penzi la dhati! Unajua kitakachotokea? Kama si kuambulia kipigo, basi utafukuzwa nyumbani kwa mwanaume huyo. Yote hayo ya nini?
BAKI NA HILI
Kamwe usijaribu kuingia katika mkumbo huu, mkumbo wa kuingia kwenye uhusiano ukiwa na uhakika huna mapenzi ya dhati. Ni jambo gumu ambalo huweza likaharibu maisha yako kabisa.
Tambua thamani ya mapenzi kwa kuheshimu hisia zako za ndani. Unapoamua chochote kuhusu mapenzi ujue unaamua jambo linahusu maisha yako.
Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Mambo ya Mapenzi anayeandikia magazeti ya Global Publishers. Ameandika vitabu vya True Love, Let’s Talk About Love na Who is Your Valentine vilivyopo mitaani.

 

ATHARI ZA KUFANYA MAPENZI MARA KWA MARA



Wapenzi wengi hasa wale ambao uhusiano wao ni mchanga hupenda sana kufanya mapenzi kila wanapokutana au wanapohisi wamehemkwa na miili yako.

 Katika hali ya kawaida kufanya mapenzi kuna faida nyingi, lakini linapokuja suala la kuzidi kiasi tunapata matatizo ya msingi ambayo huleta madhara kwa watu wanaoendekeza sana ngono.

Kuna watu ambao hawezi kulala bila kufanya mapenzi na huku wengine wakikosa uwezo wa kuvumilia hata kwa siku mbili au tatu. 

 Mtu anaweza kuwa na mke na kujikuta kila siku anatumia ‘chakula cha usiku’ kwa sababu tu hakuna wa kumkataza na kwamba ana haki ya kufanya hivyo kwa sababu amelipa mahari.

Hilo linaweza kuwa jambo jema kwa upande mwingine, lakini uchunguzi unaonyesha kuwa watu wengi kati ya watu wanaolalamika kupoteza hisia za kimapenzi hutoka katika kundi la watu wapenda ngono.

 Pamoja na tatizo hilo, yapo madhara mengine mengi ambayo mtu asiyekuwa na kiasi katika tendo la ndoa anaweza kukabiliana nayo, hivyo ni vema tukajifunza ili tusiwe watu wa kuendekeza miili kiasi cha kulazimika kufanya mapenzi kila tunapokutana hata kwenye nguzo ya umeme na chini ya miti kwa vile tu miili imetaka kufurahika.

 KUPOTEZA HAMU YA TENDO
Watu wenye pupa za kufanya mapenzi hupoteza haraka hisia za kimapenzi kwa wapenzi wao kutokana na sababu za kisaikolojia zinazoweza kujitokeza wakati wa ufanyaji wa tendo la ndoa mara kwa mara.

 Sababu hizo zinaweza kuwa ni pamoja na zile za kumzoea mwenza kiasi cha kukosa msisimko hata anapomuona akiwa mtupu.



 Aidha kukinai haraka staili za kimapenzi  kunatajwa kujitokeza kutokana na kukutana mara kwa mara kwa aina zile zile za mapenzi na pengine sehemu moja, kitanda kimoja na chumba kile kile, jambo ambalo linaweza kumfanya mhusika asione jipya kutoka kwa mwenza wake na hivyo kupoteza hamu naye na kuhisi kama hawezi tena kushiriki tendo la ndoa kikamilifu.

 KUUJAZA MWILI TAMAA KUBWA
Tabia ya kufanya mapenzi mara kwa mara huongeza uzalishaji wa homoni mwilini na kuufanya mwili uwe na msukumo mkubwa wa kutaka kuridhishwa kwa tendo la ndoa bila kukosa na hivyo kumfanya mhusika asiwe mtu mwenye uwezo wa kuzuia tamaa na kukosa chaguo la nani wa kufanya naye mapenzi na kwa wakati gani

 Watu wanaojiendekeza katika kufanya mapenzi mara kwa mara ndiyo wale ambao kila wanayemtazama barabarani humtamani bila kujali hadhi yake. 

Hawa ndiyo wanaobaka, kusaliti ndoa zao hata kwa watumishi wa ndani au kufanya mapenzi na watoto wao wa kuwazaa kwa vile akili zao huwa zimeathirika kwa tamaa ya mapenzi. 

Unapokuwa mtu wa kufanya mapenzi mara kwa mara huwezi kuwa na uwezo wa kuzuia tamaa yako. Mumeo akiondoka siku mbili unatamani kuwa hata na houseboy ili akukate kiu ya penzi. 

 KUPOTEZA RAHA KAMILI YA TENDO
Raha ya tendo hutegemea sana hisia iliyokuzwa kutokana na mapenzi sahihi na kiu ya kufanya mapenzi, hivyo basi ukiwa mtu wa kufanya mapenzi kila mara unaweza kupoteza msisimko wa tendo na kujikuta unapata furaha ambayo haikutoshi kumaliza tamaa yako.

 Kama ni mapenzi utakuwa unayafanya kwa mazoea tu na msisimko wako utakuwa mdogo!

 KUPOTEZA NGUVU ZA MWILI
Madhara mengine yanayoweza kupatikana kwa kufanya mapenzi mara kwa mara ni pamoja na kupoteza nguvu nyingi za mwili. 

Kama tujuavyo tendo la ndoa hasa kwa wanaume huwafanya watumie nguvu nyingi, hivyo kuufanya mwili uchoke. 

Aidha lishe inapokuwa ndogo kwa wafanya mapenzi mwili hukosa nguvu za kutosha kuhimili misukosuko ya kimaisha.

 Sambamba na hilo mbegu za uzazi zinazotoka kwa wanaume wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa dhaifu.

 KUPATA MAGONJWA
Kama tulivyojifunza kuwa watu wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa na tamaa na hujikuta wanafanya mapenzi holela ambayo huweza kuwasababishia magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi.

Ufanyaji wa mapenzi usiokuwa na msukumo wa kutosha hasa kwa wanawake huwafanya waishiwe msisimko na kuzifanya sehemu zao za siri kutotoa ute unaoweza kuwakinga na michubuko wakati wa kujamiiana na hivyo kuwasababishia michubuko itakayoweza kuleta maambukizi ya haraka ya magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi.

 Baada ya kungalia madhara hayo machache ni vema kwa wapenzi kupunguza kiwango cha kufanya mapenzi ili kuifanya miili iwe na uvumilivu unaoweza kumsaidia mtu kukaa kwa muda mrefu bila kumsaliti mpenzi wake hata kama atakuwa amesafiri mbali naye kimasomo, kikazi au kibiashara.

 

Makosa katika mapenzi..

 
KUNA watu wanaanzisha mapenzi, kabla ya yote tayari wanazungumza kwamba katika uhusiano wetu tutakuwa hivi na vile, lakini kuna mwingine unamwambia tu unampenda, dakika tano zijazo tayari mnakwenda kukutana faragha.

Wapo watu hawajihurumii kufanya mambo kama haya pasipo kujiuliza huyu ninaye ili awe nani.

Kuna wengine ngono wanaona kama kwenda haja ndogo na kurudi, si suala linalohitaji staha au mazungumzo ya kina kuhusu hatma yenu.

Je wewe ukoje? Ni vizuri kujiheshimu. Usijirahisi, onyesha msimamo. Usiwe mwepesi kuugawa utu wako ili umfurahishe huyo uliyenaye.

Wengine wanatoka kwao wakijua kwamba wana wapenzi, lakini wakifika sehemu za kazi, wanajirahisi, huyu akimtaka anakubali, hana msimamo, haya si maisha. Kama huyu mfanyakazi mwenzako, bosi wako anakutaka, je, kawataka wangapi? Hili ni jambo la kujiuliza.

Wengi kati ya watu wa aina hii huachwa kwa visa. Ni kwa sababu wanaonekana ni watu wasio na misimamo kwa hiyo humthamini.

Mnaweza kuachana kwenye nyumba ya wageni, au unaweza siku unampigia simu mwenzi wako mliyekubaliana mkutane sehemu fulani, haji kwa wakati. Ni kwa sababu anakuona hufai.

Haiwezikani mwanamke kweli mwenye kujiheshimu, unamtongoza saa moja na nusu, saa mbili kamili mko kwenye nyumba ya wageni.

Tena wengine unaweza kuanza kwanza kutafuta sehemu ya kumpeleka kabla ya kumhitaji, ni kwa namna tu anavyoonekana hajijali utu wake.

Kuna simulizi moja ni ya kweli, dada mmoja mrembo alikwenda baa kunywa, akakukatana na mwanamume, wakazungumza na kukubaliana waende nyumba ya wageni siku hiyo, lakini wakiwa chumbani mwanamke alidanganya anakwenda chooni, hakurudi, alikimbia.

Simulizi nyingine inahusu msichana aliyetongozwa na kujibu kuwa anachohitaji yeye ni mtu ambaye atakuwa mume na yeye awe mke? Aliendelea na msimamo huo hata baada ya kubembelezwa sana.

Je, kama wewe ni mwanamume ungeoa yupi kati ya hawa? Katika hali ya kawaida, mwenye busara angeoa huyu ambaye ameshikilia msimamo. Kwa sababu ni wazi hata baada ya kuoana atakuwa na msimamo.

Ninachotaka kusema hapa ni kuwa wengi wanaachana kwa visa kwa sababu anaona hana njia nyingine hasa kwa sababu labda anang�ang�aniwa na mtu ambaye hakuwa na sifa.

Japo watu wengine wanaachana labda kwa sababu amepata mwingine, lakini walio wengi wanaachana baada ya kubaini kuwa fulani hamfai.

Wengine pia huachana kwa sababu tu amepata mwingine, ambaye anaamini ni bora zaidi, ingawa wakati mwingine baada ya kujuana kwa kina, anaweza kuwa ni mbaya zaidi ya yule aliyetaka kumuacha.

Ndugu, kama ambavyo huyo uliyenaye zamani ulikuwa ukimuona mzuri na sasa unamuona mbaya, huwezi kujua kuhusu huyu ambaye unataka kuwa naye baada ya kumuacha huyo wa sasa.

Ndipo huwa nashauri kuwa wakati mwingine kama uliyenaye si mbaya sana, ni vizuri mkaendelea kuwa naye. Mambo yanaweza kurekebishika na kuwa safi.

Fanya hivi hasa kama rekodi yake haionyeshi kuwa ni mtu mbaya, mfano kama mtu aliwahi kuwa na mke au ana mtoto lakini hamjali, huyo kama umeoana naye na ikatokea mmeachana, ni makosa makubwa kurudiana naye.

Dalili zinaonyesha ni mtu asiyefaa, ni vigumu kuishi vizuri hata kama mtarudiana.

Kimsingi ni vigumu kuishi vizuri na mtu ambaye tayari mliachana kisha mkarudiana.

Tafiti nyingi kuhusu jambo hili zinaonyesha kwamba ni vizuri kama tayari mmeachana na mtu, kila mmoja akaendelea na hamsini zake.

Wengi wa wale wanaorudiana hali ya mahusiano yao huwa ni mbaya zaidi ya zamani, hasa baada ya miaka miwili tangu kurudiana kwao. Kama ni visa huwa ni zaidi.

Ninachotaka kusisitiza katika mada hii ni kwamba haijalishi una mwingine anayekushawishi kuachana na huyo wa sasa, au humtaki tu fulani, ni vizuri kuachana pasipo visa.

Hakuna sababu ya kuanza kumtangaza huyo mwenzi wako vibaya kwa watu ili tu aonekane ni mbaya, wakati pengine si mbaya, ila unataka kuachana naye kwa sababu zako.

Ndugu zangu hapa duniani tunapita, hakuna sababu ya kutendeana mambo mabaya. Jitahidi kuwa wazi, mwambie ukweli kwamba kweli nilikupenda, lakini hatuwezi tena kuwa pamoja kwa sababu hizi na zile.

Ni kweli ataumia, lakini ipi ni bora kuendelea na visa, au kumueleza wazi ajue moja, kama ni maumivu ya mara moja, iko siku yataisha. Ni vizuri kuelezana ukweli.

Lakini jambo moja la kujua ni kwamba ikiwa unamuacha mtu kwa sababu tu ya kumnyanyasa, hana kosa lolote, unaweza kupata mtu ambaye atakuja kuwa mbaya kuliko yule ambaye umemuacha kwa kumuonea wakati anakupenda.

Kuacha mpenzi kwa sababu zisizo na maana, ni kujitafutia laana.

Ili kuepukana kuachana ni vizuri kabla ya kuanzisha uhusiano kujuana kwa kina, ridhika na nafsi yako kabla ya kuamua.

Zungumzeni kuhusu dini, maana wengine wanakaa weee baada ya muda ndipo wanaanza kusema, eeeh bwana dini yetu si moja, ndugu wamekataa tusioane. Siku zote mlikuwa wapi kuzungumzia hili?

 

Unahitaji mwenzi wa kufa na kuzikana? Soma muongozo huu



 
Ni njia gani za kumpata mwenzi wa maisha yako? Inawezekana unakabili mtihani mzito, hujui ni yupi wa nafsi yako. Bila shaka unamtaka yule wako wa kufa na kuzikana.

Mada hii inakuja na suluhisho mahsusi kwako, kumjua mapema anayekufaa, anayeweza kudumu nawe maishani. Zingatia kwamba mwenzi sahihi wa maisha yako ni hatua muhimu kuelekea kwenye mafanikio.

KWANZA TAMBUA HILI
Uhusiano wa kimapenzi ni suala binafsi. Kwanza kabisa ni sanaa inayokutaka uangalie mahitaji yako mwenyewe. Je, unahitaji nini kwa mtu ambaye ungependa awe mwenzi wa maisha yako?

Yale unayotaka kutoka kwa mtu ambaye unapenda awe mwenzi wa maisha yako, unapaswa kuyapa kipaumbele. Hata siku moja, usithubutu matamanio ya mwili na moyo yakupe mwongozo wa kumwona umpendaye.

NANI MWENZI WA MAISHA?
Ni swali ambalo unapaswa kujiuliza. Kwa uwazi kabisa, unatakiwa kuzingatia kuwa mwenzi wa maisha ni yule ambaye utachangia naye mambo mengi kwa uaminifu na maelewano makubwa.

Mwenzi wa maisha si mtu unayeweza kuwa naye kwa mantiki ya kupeana tulizo la ngono unapohitaji au kampani ya kwenda kuangalia ‘muvi’, muziki, ufukweni na kwingineko unapoona huhitaji kuwa peke yako.
Mwenzi wa maisha ni yule atakayefanya ujione umekamilika, bila kujali ‘ubize’ wala ukapa ambao pengine unao ndani ya jamii inayokuzunguka.

Kingine cha kuzingatia ni kwamba, mwenzi wa maisha yako ni yule ambaye anakukubali na kukupenda kama ulivyo, bila kuwepo kwa nyongeza ambazo zitatokana na kukubadilisha kutoka yule wa zamani.

Kupata mwenzi wa maisha mwenye sifa kamili, ni sawa na kupatia herufi ya mwisho kwenye mchezo wa kubahatisha. Kwa maana hiyo, baada ya kumpata, kila kitu kinakuwa kimekamilika maishani mwako.

NANI MWENZI WA MAISHA YAKO?
Pointi ya msingi kuzingatia ni kwamba unahitaji kuwa na yule anayekubalika ndani ya nafsi yako. Hivyo basi, fikiria kwa yale yanayoweza kukufanya uwe na furaha, pia yanayoweza kukupa huzuni.

Zingatia mapitio yako ya nyuma kuona ni kwa namna gani yamekutengeneza mpaka kufika ulivyo sasa. Jiulize pia kuhusu ndoto na malengo yako siku za usoni.

Ikiwa tu utaweza kutambua mahitaji na matarajio yako ya kimaisha, bila shaka utaweza kutambua ni mtu gani anayefaa katika kukusaidia kutimiza kila kilichomo ndani ya malengo yako.

JENGA IMANI
Kutafuta mwenzi wa maisha siyo suala la kuangalia mtu wa kwenda naye klabu kujirusha usiku. Vile vile ni muhimu kutambua kwamba inaweza kukuchukua muda kupata mtu wa kukidhi vigezo vyako.


Pamoja na ukweli huo, bado unatakiwa uwe na imani kwamba itafika wakati utasahau habari za kutafuta mwenzi na utakuwa mwenye furaha, ukijipongeza kwa kumpata anayekufaa.

Mapenzi ni mchezo lakini ni rahisi kuucheza ukitambua kanuni zake. Hii ina maana kuwa unapokuwa kwenye kipengele hiki, unakuwa na jukumu moja zito la kuhakikisha unampata yule mwenye uwezo wa kukonga moyo. Mwenye sura ya kutimiza malengo yako.

Hata hivyo, muhimu kwako ni kuwa mtulivu na kuacha macho yafanye kazi ya kuangaza kwa utaratibu, halafu akili ifanye kazi ya kutathmini kiwango cha huyo atakayeonwa.

Kitu kingine ambacho unatakiwa kuheshimu ni kuwa, wawili wanaopendana, kila mmoja kwa nafasi yake ni nusu ya kitu kizima kinachoitwa ndoa au wapenzi, hivyo wanapounganishwa ndiyo kinapatikana kitu kizima.

Ukiamini kuwa wewe ni nusu na utakamilika baada ya kukutana na mwenzi wako, unachotakiwa kufanya ni kujenga imani kwamba mwenzi wako yupo sehemu kwa ajili yako, hivyo endelea kumtafuta na siku moja utamuweka mikononi mwako.

 

Dalili 10 za mwanaume anayekupenda.


ANAVYOTAZAMA
Mwanasaikolojia Zick Rubin kutoka Chuo cha Havard nchini Marekani aliwahi kusema kwamba watu wanaopendana hutumia asilimia 75 kutazamana kuliko wasiopendana, ambao kiwango chao ni asilimia 30-50.

Hii ina maana kwamba mwanaume anapotumia muda wake mwingi kumtazama msichana na kugeuka taratibu kuangalia vitu vingine kama mtu asiyependa kuacha kumwangalia, ujue anampenda.

MIPANGO
Mwanaume anayekupenda atakushirikisha kwenye mipango yake hasa ya muda mrefu. Mfano akitaka kununua kiwanja, kujenga nyumba atakuambia na pengine kutaka mchango wako wa hali na mali katika kulifanikisha hilo. Ukiona mwanaume anakuficha mambo yake, tambua kuwa huyo ana walakini kwenye penzi la dhati na la muda mrefu.

ATAONESHA HUZUNI
Katika maisha ya mapenzi kuna wakati wa kuhuzunika. Mwanaume mwenye upendo wa dhati atashirikiana nawe wakati wa huzuni na kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa unapata furaha.

ATAKUAMINI
Dalili nyingine ya kupendwa na mwanaume ni kuaminiwa kwenye maisha kwa ujumla. Yaani mwanaume anayekupenda hatakuficha kitu, mfano pesa zake, atakupa uhuru kwenye simu yake na kukuamini katika usimamizi wa miradi yake.

ATAKUPA NAFASI
Ninapozungumzia nafasi nina maana atakukaribisha kwake bila hofu na kukupa nafasi ya kuingia na kutoka bila mipaka, atakupa nafasi ya kuweka vitu vyako kwenye kabati na kuruhusu nguo, picha na vitu vyako kuonekana wakati wote chumbani kwake.

UTAKUWA MWANAFAMILIA
Mwanaume aliyefikia chaguo la mwisho kwa mwanamke humshirikisha mpenzi wake kwenye masuala yake ya kifamilia, mfano atamwalika kwenye vikao vya harusi, kipaimara, atatoa nafasi ya kuambatana naye kuona wagonjwa, kusalimia ndugu na atakuwa huru kukutambulisha kwao.

ATAZUNGUMZA NAWE KUHUSU WATOTO
Kwa kuwa wanaume wengi hufikiria kuwa na familia, mwanaume anayekupenda atazungumza nawe mipango ya kupata watoto kwa kuwa atakuwa amekuchagua wewe kuwa mama wa wanaye na atapenda mazungumzo hayo.

ATAKUSAIDIA
Kwa kuwa kukwama ni sehemu ya maisha yetu, mwanaume anayekupenda atakuwa tayari kukusaidia unapokwama. Kila mara atahakikisha kuwa unakuwa na mafanikio na yeye atakuwa tayari kukupunguzia usumbufu wa maisha, kwa kukufuata kazini, kukusaidia baadhi ya mambo na hata ya nyumbani.

ATAJITOLEA
Ninaposema kujitolea ninamaanisha atakuwa tayari kufanya mambo yako na kuyaweka yake nyuma. Kwa mfano akiwa anapenda mpira na siku hiyo kuna mechi, lakini muda huo ukamwambia akufuate kwa mjomba wako atakuwa tayari kuacha furaha yake na kukujali wewe. Huyu ni mwanaume anayekupenda kwa dhati.

ATAAMBATANA NAWE
Wapenzi wengi wasiokuwa na mapenzi ya dhati huona aibu kuambatana na wapenzi wao kwenye mikusanyiko ya watu, lakini mwanaume anayekupenda atafurahia kutoka moyoni kuongozana nawe kwenye halaiki ya watu na kufurahia uwepo wako bila kuona aibu.

Mada hii inaishia hapa, hebu jiulize mwanadada, huyo uliyenaye anakufanyia haya, kama sivyo kwa kiwango kikubwa utakuwa na kazi ya kuhakiki penzi lako na pengine kujenga misingi mipya ya uhusiano wenu kabla haujavunjika.

 

NJIA SAHIHI ZA KUACHANA NAMWENZI WAKO

Unapotaka kupeleka ujumbe kwa mpenzi wako kuwa hayuko tena moyoni mwako, lazima tu ujitolee kupata hasara katika baadhi ya mambo. Kumbuka kuwa huhitaji tena uhusiano na mwenzako.
PUNGUZA MWITIKIO WAKE
Kuna wakati ambapo rafiki au mpenzi wako atafanya au kusema jambo na wewe utatakiwa kuonesha mwitikio. Kama umeshadhamiria kuachana naye, onesha mwitikio wa shingo upande.
Kama mhusika atabaini jinsi ulivyoitikia shingo upande, utakuwa umepeleka ujumbe maridhawa, kuwa huna tena furaha na uhusiano wenu na kwamba unahisi ni wakati muafaka wa kumaliza mambo.

Kuna mazingira ambayo hutaepuka kumwitikia mpenzi au rafiki unayetaka ‘kumpiga chini’. Kwa sababu hiyo, ndiyo maana unapaswa kumwitikia lakini katika hali ambayo inaonesha kwamba huna habari naye tena.

Unapomwitikia mpenzi wako kwa shingo upande, unamwonesha kuwa yeye siyo kipaumbele kwako, jambo ambalo litamfanya kuona kuwa yamkini ni wakati muafaka wa kupunguza moto wake kwako.

PUNGUZA UKARIBU NAYE
Kama umekuwa na mazoea ya kuwa karibu na mpenzi wako kama ilivyo kawaida, anza kujenga mazingira ya kujitenga naye mnapokuwa mbele za watu ili aweze kuhisi mabadiliko katika mwenendo wako.
Haina maana kuwa usizungumze naye, kaa naye karibu na uzungumze naye kama kawaida, lakini majibu yako yawe ya mkato.  Pia usikae karibu naye sana, maana namna hiyo utalazimika kuzungumza naye na kukaribisha lugha yake ya matendo.

Lakini kama itawezekana, jishughulishe zaidi kuzungumza na watu wengine ili kwa kiasi fulani huyo mwenzako aweze kuona kuwa hukumpa kipaumbele cha kwanza.
ONESHA WATU KWAMBA HAUPO NAYE
Bila kulazimika kumfedhehesha mwenzako, chukua hatua za kuuonesha umma unaowazunguka kuwa yeye si tena mdau muhimu katika maisha yako, mathalani kwa kutomwalika kwenye shughuli muhimu ambazo ulizoea kumwalika. 
Unapolazimika kumwalika, weka mipaka katika mazungumzo yako na yeye. Hata hivyo, haishauriwi kuwatangazia marafiki zako wengine kuwa unataka kumtenga mpenzi au rafiki yako huyo, maana namna hiyo watajiwa na fikra kuwa yamkini ana matatizo kumbe kwa hakika kama kuna mwenye matatizo basi ni wewe (au unavyopaswa kuwafanya watu waamini).
Kama unataka kuwa mstaarabu, hakikisha kuwa hakuna mtu mwingine anayeingia katika mchakato huu wa kumbwaga mpenzi au rafki yako, kwani hii ni suala lako binafsi.

USIJIBEBESHE MZIGO
Hakuna haja ya kubeba mzigo wa uhusiano ambao huna maslahi nao. Japo baadhi ya wanawake huwalalamikia wanaume ambao huwachezea kisha wakawaacha, ukweli ni kwamba hupaswi kuendelea na uhusiano ambao haukupi kile ukitakacho.
Watu wengi walishafanya hivi na kufanikiwa kumaliza vema uhusiano wao na wapenzi wao. Hakuna ubaya wowote kufanya hivi pale unapoona kuwa mwenzako anakupeleka kule ambako usingependa kwenda kwa sasa.
Iwapo utatokea mgogoro wowote au mpenzi wako akawa na malalamiko, bahati nzuri tayari unazo sababu zako ambazo umetakiwa kuziweka bayana mawazoni. 
Hapo ndipo utakapozianika mbele yake na kumweleza msimamo wako mpya. Hata hivyo, utaratibu huu wa kumaliza uhusiano unafaa zaidi kwa wapenzi ambao mahusiano yao hayajajenga mizizi au wale ambao ni marafiki wa kawaida.
Kama uhusiano wako na mwenzako umeshaota mizizi, zipo tahadhari nyingi zaidi za kuchukua, maana ulishampotezea mwenzio muda mwingi.

 

fanya haya! Unapotokea kumpenda mtu aliye na mpenzi wake,.




Tumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ametuwezesha kuonana tena wiki hii tukiwa wazima. Lakini pia tumshukuru kwa kutuletea kitu kinachoitwa mapenzi.

Mapenzi yamekuwa yakichukua nafasi kubwa sana katika maisha yetu ya kila siku na yamekuwa yakichangia kwa kiasi kikubwa furaha kwa kila mtu.

Kama huamini, angalia wale waliotokea kupenda na wao wakapendwa, utabaini nyuso zao zimetawaliwa na furaha isiyo na kifani. Lakini mapenzi hayo hayo yamekuwa ni chanzo cha vilio kwa baadhi ya watu.

Mpenzi msomaji wangu, kupenda hakuna macho! Moyo ukishapenda hausikii la kuambiwa. Katika hili ndiyo maana unaweza kumuona mwanaume kazimika kwa demu ambaye hawaendani kabisa lakini moyo wake ndiyo umeshapenda.

Ilishawahi kutokea msichana akampenda kijana mmoja ambaye ni fukara kupita maelezo. Yeye akawa ndiyo anamhudumia kwa kila kitu. Akamfanyia mpango wa ajira na mwisho wake wakafunga ndoa.

Sasa hivi wanaishi maisha ya furaha na amani. Wamegeuka mfano wa kuigwa kwa jinsi wanavyopendana lakini huko nyuma msichana huyo alikuwa akichekwa kwa kutoa penzi kwa mwanaume asiye na mbele wala nyuma.

Hayo ndiyo mapenzi jamani! Lakini pia katika kufurukuta kumtafuta mpenzi wa kuwa naye maishani, mwanaume anaweza kujikuta unaangukia kwa demu ambaye tayari ana mpenzi wake.

Moyo wako unakuambia yeye ndiye mtu sahihi katika maisha yako lakini tayari ana mtu wake, unafanyaje?

Utapambana kuhakikisha unapata kile ambacho moyo wako umekipenda au utakubaliana na ukweli kwamba huwezi kuwa naye kwa kuwa ana mtu wake? Inapofikia hatua hiyo unaweza kujikuta upo njia panda hasa pale ambapo huyo mwenye mtu wake naye anaonesha kuwa na chembechembe za mapenzi kwako.
Kuna mambo kadhaa ya kukusaidia kukabiliana na hali hii.

Chunguza
Tumia muda wako mwingi kuchunguza juu ya uhusiano wake. Uhusiano wao umesimama na wanaonekana ni watu wenye ‘future’? Nasema hivyo kwa sababu, yawezekana uhusiano wa huyo uliyetokea kumpenda ni wa kuzuga tu na huenda wewe ndiye mwenye ‘future’ naye. Ndiyo maana nikasema chunguza uhusiano wake kwanza.

Usitafute uadui
Baada ya kuchunguza, ukibaini kwamba uhusiano wao hauko ‘siriasi’, vuta subira, lolote linaweza kutokea na likaufurahisha moyo wako. Lakini kama utaona ni watu walio siriasi na wanaelekea kuoana, usitafute uadui bure, kaa pembeni.

Una nafasi kwake?
Sawa umetokea kumpenda msichana aliye na mtu wake, umeshawahi kujiuliza kama una nafasi ndani ya moyo wake? Anaonesha dalili fulani za kukupenda kama unavyompenda na ni mtu anayeonesha kukumisi anapokuwa mbali na wewe? Utakapobaini una nafasi kwake, uamuzi wa kumpotezea hautakuwa na nafasi.

Ni rahisi kubadili uamuzi wake?
Unadhani huyo uliyetokea kumpenda anaweza kubadili maamuzi ya kumuacha huyo aliyenaye kama kweli hawana ‘future’? Utagundua hilo kwa kuongea naye na kumsikia kama anaweza kufanya maamuzi hayo ili awe na wewe.

Pingana na moyo wako
Ifike wakati upingane na moyo wako. Unajua moyo wako kukuambia kuwa unataka kuwa na uhusiano na demu ambaye tayari ana mpenzi wake wakati mwingine utakuwa unakupotosha.

Kwa hiyo ukiona vipi, pingana nao. Acha kumng’ang’ania msichana mwenye mpenzi wake licha ya ukweli kwamba, huenda wewe ndiye mwenye nafasi ya kuwa mume wake na siyo huyo aliye naye.

Urafiki ni poa?
Umempenda sana na hauko tayari kumkosa katika maisha yako lakini imetokea kwamba tayari yuko na mtu na umebaini huna nafasi kwake kabisa? Usiumie, omba angalau urafiki. Siyo urafiki wa kivile sana ila angalau pale unapotaka kusikia sauti yake kwa kumsalimia tu, upate nafasi hiyo.

Usiumie, yupo mwingine
Haina haja ya kujitafutia vidonda vya tumbo bure kwa kuwa tu umebaini uliyetokea kumpenda tayari ana mtu. Chukulia ni hali ya kawaida, mademu wazuri ambao wanaishi singo wapo kibao huko mtaani, ni suala la wewe kutulia tu. Amini yupo mwingine ambaye atayafanya maisha yako yawe ya furaha.

Naomba nihitimishe kwa kusema kwamba, unapotokea kumpenda mtu fulani, pambana kuhakikisha unampata kwa sababu ukimkosa maisha yako yanaweza kuwa gizani. Ila pale utakapoona uwezekano wa kuwa naye haupo, usilazimishe ndugu yangu. Kumbuka haya ni maisha tu!

 

Mambo ya kuzingatia unapomtumia mpenzi wako zawadi



Nazungumzia ishu ya wapenzi kununuliana zawadi. Hapa sizungumzii zawadi ambazo wengi wetu tumekuwa tukinunuliana siku za Sikukuu kama vile Iddi, Krismasi, Valentine na nyinginezo bali namaanisha zawadi nje ya siku hizo.
Kumtumia mwenzi wako zawadi ni kati ya mambo ambayo humfanya afurahie uhusiano wake na wewe. Hata hivyo, hakuna zawadi za moja kwa moja ambazo ni rasmi kwa ajili ya wapenzi lakini ni vyema ukamtumia zawadi kulingana na mapenzi yake zaidi.
Kwa kuwa wewe unamfahamu zaidi mwenzi wako, unaweza kujua zawadi gani ni nzuri zaidi kwake au anayopendelea kuliko aina nyingine.
Wiki hii nimechambua aina kuu za zawadi ambazo ukimtumia mpenzi wako utamteka hisia zake na ataona unamjali.
Mavazi
Mavazi ni kati ya zawadi ambazo zitamfanya mpenzi wako azidi kukupenda na kuwa karibu zaidi na wewe.
Aina ya nguo ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako ni zile ambazo unaamini atavutiwa nazo au zile ambazo zitampendeza na kumfanya aonekane nadhifu.Hata hivyo, zipo aina za mavazi ambazo zimependekezwa zaidi kwa ajili ya wenzi kutumiana wanapokuwa mbali na hata wanapokuwa karibu.

Kama wewe ni mwanamke unataka kumtumia mpenzi wako wa kiume, mavazi yafuatayo yanafaa zaidi. Saa nzuri ya mkononi, nguo za ndani, lakini lazima uzingatie rangi ya bluu, bluu bahari au nyeupe kimsingi zisiwe za rangi zinazoficha uchafu.

Zingine ni fulana za ndani ‘singlendi’, fulana, mkanda wa suruali, simu ya mkononi, vitambaa vya jasho n.k. Hakikisha katika zawadi hizo, unaambatanisha na manukato mazuri hasa yale ambayo unajua atayapenda.
Haishauriwi kumtumia suruali au shati kwa sababu inaweza kuwa kubwa au ndogo, hivyo kupunguza ladha ya zawadi hasa kama atakuwa ameipenda sana.

Zawadi za aina hiyo, unaweza kumpa mwenzi wako ofa ya kwenda kuchagua moja kwa moja dukani lakini kama unajua saizi yake na una uhakika akivaa atapendeza, ruksa kumnunulia vitu hivyo na tena utakapopatia saizi yake vizuri ataamini uko makini naye na unampenda kwa dhati.

Kama wewe ni mwanaume na unataka kumtumia mpenzi wako wa kike zawadi, lazima uwe makini sana! Mavazi yaliyopendekezwa hapa ni pamoja na batiki (gauni, blauzi na sketi, blauzi yenyewe n.k), hereni, bangili, mkufu, simu ya mkononi, saa ya mkononi, nguo za ndani (kulingana na mapendekezo yake, kwa jinsi umjuavyo), sidiria, viatu n.k.
Kama umesoma vizuri utaona mwanamke anaweza kununuliwa vitu vingi zaidi (hasa nguo) tofauti na mwanaume. Hii inatokana na aina za mavazi na saizi zao kukaririka kirahisi zaidi au kutokuwa na saizi ya moja kwa moja. Mathalan, batiki, sketi na blauzi na vinginevyo. Kama kawaida, mavazi haya, ambatanisha na manukato mazuri, hasa yale ambayo ndiyo anayopendelea mpenzi wako.
Maua pia ni kati ya zawadi zinazopendekezwa na wataalamu wa mambo ya mapenzi. Maua ni mazuri sana kwa mwezi aliye mbali, lakini ni vyema kuzingatia na umbali uliopo kati yenu, kwani maua huweza kusinyaa kabla ya kumfikia (hasa kama ukimtumia yale halisi, kwani ndiyo haswa mazuri).

Hata hivyo, zipo zawadi nyingine ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako kwa kuangalia vitu anavyovipenda sana.
Hii ni njia pekee ya kuonesha ubunifu wako na jinsi unavyomjali hata akiwa mbali kwa kumtumia vitu ambavyo huwa anavipenda lakini alipo hawezi kuvipata!
Mathalan, mpenzi wako anapenda sana zabibu lakini amekwenda mkoa ambao vitu hivyo havipatikani kwa urahisi, hii ni nafasi yako kumtumia.
Mathalan unajua kabisa anapenda sana kusoma vitabu lakini sehemu aliyopo hawezi kupata, basi nunua majarida, magazeti na matoleo yote ambayo hajayapata kisha mtumie, hakika utakuwa umemfurahisha sana na kumfanya afurahi kupata vitu hivyo.
Kwa leo naomba niishie hapo, lengo ni kukufahamisha kwamba zawadi ni kitu muhimu sana katika kuliboresha penzi lenu. Kwanza mpenzi wako aamini kwamba unampenda lakini pia unamjali.

Nazungumzia ishu ya wapenzi kununuliana zawadi. Hapa sizungumzii zawadi ambazo wengi wetu tumekuwa tukinunuliana siku za Sikukuu kama vile Iddi, Krismasi, Valentine na nyinginezo bali namaanisha zawadi nje ya siku hizo.
Kumtumia mwenzi wako zawadi ni kati ya mambo ambayo humfanya afurahie uhusiano wake na wewe. Hata hivyo, hakuna zawadi za moja kwa moja ambazo ni rasmi kwa ajili ya wapenzi lakini ni vyema ukamtumia zawadi kulingana na mapenzi yake zaidi.
Kwa kuwa wewe unamfahamu zaidi mwenzi wako, unaweza kujua zawadi gani ni nzuri zaidi kwake au anayopendelea kuliko aina nyingine.
Wiki hii nimechambua aina kuu za zawadi ambazo ukimtumia mpenzi wako utamteka hisia zake na ataona unamjali.
Mavazi
Mavazi ni kati ya zawadi ambazo zitamfanya mpenzi wako azidi kukupenda na kuwa karibu zaidi na wewe.
Aina ya nguo ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako ni zile ambazo unaamini atavutiwa nazo au zile ambazo zitampendeza na kumfanya aonekane nadhifu.Hata hivyo, zipo aina za mavazi ambazo zimependekezwa zaidi kwa ajili ya wenzi kutumiana wanapokuwa mbali na hata wanapokuwa karibu.

Kama wewe ni mwanamke unataka kumtumia mpenzi wako wa kiume, mavazi yafuatayo yanafaa zaidi. Saa nzuri ya mkononi, nguo za ndani, lakini lazima uzingatie rangi ya bluu, bluu bahari au nyeupe kimsingi zisiwe za rangi zinazoficha uchafu.

Zingine ni fulana za ndani ‘singlendi’, fulana, mkanda wa suruali, simu ya mkononi, vitambaa vya jasho n.k. Hakikisha katika zawadi hizo, unaambatanisha na manukato mazuri hasa yale ambayo unajua atayapenda.
Haishauriwi kumtumia suruali au shati kwa sababu inaweza kuwa kubwa au ndogo, hivyo kupunguza ladha ya zawadi hasa kama atakuwa ameipenda sana.

Zawadi za aina hiyo, unaweza kumpa mwenzi wako ofa ya kwenda kuchagua moja kwa moja dukani lakini kama unajua saizi yake na una uhakika akivaa atapendeza, ruksa kumnunulia vitu hivyo na tena utakapopatia saizi yake vizuri ataamini uko makini naye na unampenda kwa dhati.

Kama wewe ni mwanaume na unataka kumtumia mpenzi wako wa kike zawadi, lazima uwe makini sana! Mavazi yaliyopendekezwa hapa ni pamoja na batiki (gauni, blauzi na sketi, blauzi yenyewe n.k), hereni, bangili, mkufu, simu ya mkononi, saa ya mkononi, nguo za ndani (kulingana na mapendekezo yake, kwa jinsi umjuavyo), sidiria, viatu n.k.
Kama umesoma vizuri utaona mwanamke anaweza kununuliwa vitu vingi zaidi (hasa nguo) tofauti na mwanaume. Hii inatokana na aina za mavazi na saizi zao kukaririka kirahisi zaidi au kutokuwa na saizi ya moja kwa moja. Mathalan, batiki, sketi na blauzi na vinginevyo. Kama kawaida, mavazi haya, ambatanisha na manukato mazuri, hasa yale ambayo ndiyo anayopendelea mpenzi wako.
Maua pia ni kati ya zawadi zinazopendekezwa na wataalamu wa mambo ya mapenzi. Maua ni mazuri sana kwa mwezi aliye mbali, lakini ni vyema kuzingatia na umbali uliopo kati yenu, kwani maua huweza kusinyaa kabla ya kumfikia (hasa kama ukimtumia yale halisi, kwani ndiyo haswa mazuri).

Hata hivyo, zipo zawadi nyingine ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako kwa kuangalia vitu anavyovipenda sana.
Hii ni njia pekee ya kuonesha ubunifu wako na jinsi unavyomjali hata akiwa mbali kwa kumtumia vitu ambavyo huwa anavipenda lakini alipo hawezi kuvipata!
Mathalan, mpenzi wako anapenda sana zabibu lakini amekwenda mkoa ambao vitu hivyo havipatikani kwa urahisi, hii ni nafasi yako kumtumia.
Mathalan unajua kabisa anapenda sana kusoma vitabu lakini sehemu aliyopo hawezi kupata, basi nunua majarida, magazeti na matoleo yote ambayo hajayapata kisha mtumie, hakika utakuwa umemfurahisha sana na kumfanya afurahi kupata vitu hivyo.
Kwa leo naomba niishie hapo, lengo ni kukufahamisha kwamba zawadi ni kitu muhimu sana katika kuliboresha penzi lenu. Kwanza mpenzi wako aamini kwamba unampenda lakini pia unamjali.

 HAWEZI KUSEX MPAKA ASHIKE UUME

Mimi ni msichana nimewahi kuwa na rafiki wa kiume hapo nyuma, huyo kaka alikua tu kama rafikiyangu baadae ikatoke tukapendana na kuwa mtu na girlfriend wake I mean tulianza kutoka kama wapenzi.

Huyo mwanaume alikua yuko nice ingawa baadae tulikuja tukaachana. Tatizo la huyo mwanaume ni wakati wa kufanya mapenzi. 


Tulikua tukifanya romance , tukiwa tunajiandaa kufanya mapenzi alikua yuko vizuri , tu tunaendana vizuri na wote tunakua tuko tayari kungonoka ila wakati wa kungonoka ndo kasheshe linaanzia hapo.

Kwanza uume wake hauingii, yaani ni lazima ashikilie na mkono ndo aanze kuingiza na kutoa na hata kama akishikilia bado hawezi kutia kabisa yaani hawezi kwenda juu na chini na hata mimi nashindwa kumsapoti kukatika kwani uume wake unakua kama umeshasinyaana.


Kitu kingine alikua anadai eti uchi unateleza kwa hiyo ananifuta ndio aingize ukiwa mkavu kabisa wakati mimi najua uchi ukiwa una ute ndio rahisi kwa kufanya mapenzi na pia haiwi kazi ngumu kuingiza.


Uume  wake ulikuwa unaonekana umesimama sana ila hauingii unakua kama hauna nguvu. 


Huyu mwanaume alinitesa kweli kihisia kwani nilikua na ham  sana lakini ndio hivyo hawezi kuingiza nakuiacha peke yake ....lazima aishikilie na mkono na ananifuta uchi uwe mkavu ndio ajaribishe kuingiza....

Yaani  kuna mda tulikuwa tunafikia  mpaka tunaamua kuacha kwani hafanikiwi kuingiza anajishikilia kwenye kichwa anaingiza kichwa kidogo.
 Nakumbuka nimeshawahi kuwa nae siku mbili lakini alifanikiwa kuingiza mara moja na hakukaa hata dakika kumi ikatoka.

Alafu sijawahi muona akipiga  bao  zaidi ya mara moja tu .JE, hili ni tatizo gani kwa mwanaume huyu?
 

 
Ukimuangalia ni handsome, ananguvu za kutosha tu na uume  wake unasimama vizuri na ni mkubwa vizuri na isitoshe nilikuwa namfanyia blow job ya kutosha na nampa romance ya kutosha kuhakikisha yuko tayari lakini wapi.

Mwenzenu yaliyonipata ndio hayo, Ingawa yule mwanaume niliachana naye ila kila siku nimekuwa nikifikiria je hili ni tatizo gani? Nimekaa na siri moyoni lakini kwa kweli imenishinda .


Na sio kwamba umri wake ni mkubwa ni bado kijana mdogo hajafika hata miaka thelathini, kwa mnaojua labda nini atumie ili awe anajiweza kimapenzi hata nijaribu kumshauri kwani nasikia hata msichana aliyenae sasa ameshaanza kulalamika kwa watu.


Na sikupenda lile tatizo lake kwani wakati wa tendo  alikua anahangaika sana utamuonea huruma na tunaishia tu kujaribu kuingiza hatufanikiwi kufanya.

Asanteni.

USHAURI   WA TATIZO

Hili tatizo lipo kwa kiasi kikubwa sana miongoni mwa wanaume lakini kutokana na UANAMUME  huwa hawapendi kulizungumzia sio kwa wapenzi wao tu bali hata kwa madaktari.

 MTAZAMO

HUYO MTU ANATATIZO  LIITWALO  PARTIAL IMPOETANCE.
HUSABABISHWA NA VITU VINGI,WOGA WA MUNGU,WOGA WA MAHALI PA KUFANYIA TENDO,
 WOGA WA MAGONJWA,WOGA KWA MSICHANA KWA MAANA YA KUOGOPA KUUMBUKA AU KUMKAMIA SANA MSICHANA AU KWA KUTAKA KUMWOMYESHA BINTI KUWA ANAYAWEZA.

 NA MSONGO WA MAWAZO KWA UJUMLA.PIA HUTOKEA KAMA MTU HAJAMFEEL SANA MTU AU ANASUTWA NA NAFSI KWA KUTAKA KUIBA NGONO.

NYONGEZA  YA VISABABISHI.

1)-Maumbile ambayo wengi wanarithi.

2)-   Mtu  aliyezoea  kupiga punyeto kwa  muda  mrefu

3)- Matatizo ya Kisaikolojia yaliyosababishwa na wanawake (ana historia mbaya na wanawake),

3)-Kuugua kwa muda mrefu huko nyuma (matokeo ya matumizi ya dawa mbali mbali),

4)-Kutojiamini,

5)- Wewe kutokuwa "relaxed" yaani unanyege na uko mnyevu lakini pia uko "tense" hatoweza kuingia na jinsi anavyojitahidi kuingia anashindwa inampunguzia kujiamini  hata kuhisi kuchoka na kupoteza ugumu wa uume wake.

6)-Stress kutokana na maisha au shughuli za kimaisha na kazi.

7)-Kutokujua afanyacho (sio mzoefu sana) na labda anajua wewe mambo yako yako juu.

8)-Umri mdogo kitu kinachoweza kusababisha yeye kutokuwa tayari kwa tendo au kuwa kenye uhusiano wa kimapenzi na ngono......nakadhalika.

NINI  KIFANYIKE?

Kutokana na umri mdogo wa mpenzi wako huyo wa zamani sidhani kama ni busara kumshauri kutumia dawa za kuongezea nguvu zile za kisasa au za kienyeji za kiume kabla ya kujaribu njia za kawaida ambazo hazina madhara .

Njia hizo ni kujitahidi na kujua hali yake hiyo inasababishwa na nini hasa? Na hilo litafanikiwa ikiwa ataondoa aibu na kuweka pembeni "ego" yake na kwenda kumuona Daktari na kumueleza yaliyomsibu huko nyuma kama yapo(Kisaikolojia), Kinachompata anapokuwa na wewe (labda kutojiamini/uoga), amewahi kuugua alipokuwa mdogo, kuna matatizo ya kiafya kiukoo kama kisukari n.k


Sasa kwa vile hana mpenzi kwa sasa na wewe inaonyesha unampenda, unamjali na kutaka kumsaidia basi sio mbaya kama mkarudiana (sio lazima ) ukamsaidia kwa kutumia  bidhaa iitwayo "cock ring"..

  Inapatikana kwenye maduka ya dawa sambamba na Condom lakini "pete ya uume" hiyo husaidia kuufanya uume kubaki mgumu kwa kutoruhusu damu iliyojaa uumeni kushuka chini nakusababisha "kiungo" kulegea au kupoteza u-firm wake.

Kifaa hiki huwekwa chini kabisa karibu na pumbu pale uume unaposimama na kukaza hali itakayomfanya mwanaume asimamishe kwa muda mrefu kuliko kawaida yake na haina maumivu yeyote kwako wewe wala yeye mwanaume kwani bidhaa hiyo imetengenezwa kwa mpira. 

Vilevile ajitahidi kula vyakula vyene vitunguu saumu, apendelee kula vyakula vya baharini hasa pweza.

ASANTENI.


NJIA ZA KUFANYA MATITI YASILALE

http://girlstz.faa.im/files/akao.jpg

Ikiwa wewe umechelewa(ulikuwa hujui hili wakati matiti yako yanaota) basi msaidie mdogo wako au binti yako anaekuwa hivi sasa, ili asije kujisikia vibaya pale wanaume watakapokuwa wakiponda  matiti kwa kuyaita "malapa"....
http://t3.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcRyInzJORWU9bOFYf7dwycJIhIIcLAkVcE7yuopRN-63EoUIMt9dg

Kwanza kabisa hakikisha mtindo wa kulala ni kifudifudi (kulalia tumbo), kwa kufanya hivyo kunasaidia kwa kiasi kikuwa kufanya matiti yako pumzike, kwamba hakutakuwa na kuning'inia kama utakuwa umelala chali(lalia mgongo) au kiubavu.

Zoezi...1
Asimame wima dhidi ya mlango au ukuta kisha aegeshe matiti yake mahali hapo kwa nguvu kisha aachie (ajitoe ukutani), zoezi hili hufanya matiti yaume sana lakini wewe kama dada  mpe moyo kuwa avumilie. Afanye hivyo mara 20 kila asubuhi.

Zoezi....2
Simama wima huku mikono yako ikiwa imenyooshwa huku na kule kisha ipeleke mbele nakukutanisha viganja vyako alafu irudishe nyumba kadiri uwezavyo (sio lazima ikutane) ila utahisi maumivu fulani sehemu ya matiti (misuli yafanya kazi hapo)....fanya hivyo mara 10 na ongeza hesabu njinsi unavyokua.

Zoezi...3
Ukiwa umesimama wima na mikono yako imenyooshwa huku na hule inanyue taratibu kuelekea juu na kutanisha vidole vyako huko juu kisha rudisha mikono ilipokuwa (imenyooka huku na kule).