Na Imelda Mtema
MOJA kati ya sifa kubwa ya mwanamke ni 
kujua kupika. Zipo baadhi ya ndoa ambazo huvunjika kutokana na tatizo la
 mwanamke kutojua kupika.
Kwenye ulimwengu wa mastaa wa kike Bongo, wapo wengi wanaojua kupika chakula kizuri na wapo ambao hawajui.
Kizuri huwa kinajiuza siku zote, sifa 
njema huwa inazungumzwa na wengi ndiyo maana ni rahisi kuwasikia hata 
wakisifiana wenyewe kwa wenyewe pindi wanapobaini miongoni mwao yupo 
anayejua kupika zaidi.
Tathmini yangu ya kina katika safari 
zangu za kila siku kwenye tasnia ya habari, nimeweza kujifunza kuwa wapo
 mastaa ambao ni hodari kwa kupika na sifa zao zimekuwa zikikua siku 
hadi siku.
Mara kadhaa nimeshawahi kuwasikia mastaa
 wa kiume kama Jacob Steven ‘JB’, Vincet Kigosi ‘Ray’ Single Mtambalike 
‘Richie’ wakiwasifia baadhi ya wasanii wa kike ambao wanajua kupika 
vizuri.
Katika makala haya nakuletea baadhi ya 
mastaa ambao wanaongoza kwa kutajwa kuwa ni ‘mafundi’ wa kupika 
madikodiko ambapo kila mmoja ana siri yake iliyomfanya awe anajua 
kukaangiza:
Aunty Ezekiel
Huyu ni staa ambaye kwa muonekano wa nje
 anaonekana ni sistaduu anayejipenda sana na ukadhani si mtu wa kuingia 
jikoni au kujishughulisha na kazi zozote za nyumbani, lakini ni mtaalam 
wa kupika balaa.
Mwenyewe anasema alikuwa akipenda kupika
 tangu akiwa mdogo na alikuwa hodari wa kuwaangalia watu aliokuwa 
akiishi nao na kuweza kupata ujuzi wa mapishi. Ni mtaalam wa kupika 
chakula chochote na ukibahatika kula utadhani kimepikwa kwenye mahoteli 
yenye hadhi.
WEMA SEPETU
Beautiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’ 
ni hatari ukimkuta jikoni, anapokuwa jikoni siyo yule unayemuona kila 
kukicha kwenye matukio mbalimbali, anapika vyakula ambayo mara nyingi 
huwa ni vigumu kwa wanawake wengi  kama katles, kababu, Sambusa na 
vyakula vingine vingi.
Wema anasema ufundi wa jikoni aliupata 
kutoka kwa mama yake mzazi, Mariam ambaye mara nyingi anapata tenda 
kubwa za kupika vyakula sehemu mbalimbali hivyo alikuwa makini sana 
kuiba ujuzi wake.
MONALISA
Yvonne Cherry ni msanii wa kitambo. Siku
 moja nilipata bahati ya kwenda nyumbani kwao, Yombo Buza ambapo 
nilimkuta akiwa jikoni na alipomaliza na kukionja chakula chake 
nilikubali, anajua kuchanganya vitu vingi kwenye chakula na kuleta ladha
 ya aina yake.
Monalisa anasema kuwa ufundi huo 
aliupata kutoka kwa bibi yake, mama Ngatwika aliyekuwa akimfundisha 
namna ya kupika vyakula mbalimbali. 
JACQUELINE WOLPER
Yeye huwezi kujua kabisa kama ni mtaalam
 wa jikoni. Ukibahatika kumkuta jikoni basi utagundua huwa anatumia muda
 mwingi kuandaa chakula kitamu ndiyo maana baadhi ya wasanii wenzake 
wanapenda kumpigia simu na kumwambia wanakwenda kula nyumbani kwake.
Wolper anasema kuwa utaalam wa jikoni 
aliupata toka kwa mama yake kwani nyumbani kwao watoto wote bila kujali 
jinsi wanafundishwa kupika.
JOHARI
Blandina Chagula ndiyo funga kazi. Ni 
mtaalam balaa wa mapochopocho yote ambapo wasanii wenzake akiwemo Irene 
Uwoya siku zote huwa anampigia ‘saluti’ na hata zinapotokea sherehe 
ndogondogo yeye ndiyo hupewa nafasi ya kuwa msimazi wa kupika.
Mwenyewe anasema ujuzi huo ni kipaji 
alichozaliwa nacho kwani toka akiwa mdogo, alikuwa na uwezo wa kupika 
chakula cha kula watu wa nyumba nzima na kila mmoja akaridhika. 
