Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunakuwa katika uwanja mpana zaidi wa tafakari za kibaiolojia na kisaikolojia walizonazo wanaume.
Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo sehemu kuu tatu zinaweza 
kabisa kukidhi mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili linavyowasumbua 
wanaume wengi duniani.
Sehemu kubwa ya malalamiko ya wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi maeneo matatu ambayo ni KUKOSA MSISIMKO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO NA KUKOSA KABISA NGUVU,
 huku kufika kileleni mapema kukihusishwa pia kama pacha wa janga hili 
ambalo linawasumbua zaidi wanaume, ingawa na wanawake wanakabiliwa na 
sehemu ndogo ya tatizo hili.
Hata hivyo uchunguzi wa hivi karibuni uliowahusisha wanaume 
wanaofika kliniki au kupata tiba za tatizo la upungufu wa nguvu za kiume
 umeonesha kuwa, sio wanaume wengi wenye sababu za kibaiolojia 
zinazowafanya wakose nguvu za kiume, isipokuwa wengi wao huwa na 
matatizo ya kisaikolojia zaidi ambayo wahusika wanaweza kujiponya nayo 
bila hata kutumia vidonge wala dawa za miti shamba.
Ingawa Matabibu wanataja magonjwa ya moyo, kisukari, shinikizo la 
damu, magonjwa ya zinaa, unene wa kupita kiasi, umri mkubwa kuwa ndiyo 
chanzo cha wanaume kupungukiwa na nguvu za kiume, lakini imebainika kuwa
 idadi kubwa ya wanaume wanaofika hospitalini kutafuta nguvu za kiume 
hawana magonjwa hayo
Huu ni ushahidi kuwa wanaokabiliwa na janga hili wamebeba tatizo la
 upungufu wa nguvu za kiume kimawazo zaidi kuliko hali halisi.
Ukweli wa mambo ulioibuliwa na wanasaikolojia umebaini kuwa, wale 
wote wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana nguvu iwe ya kufika kileleni 
mapema, kutokuwa na msisimko na kushindwa kurudia tendo wamekosa maarifa
 tu ya kufahamu na hawaijui miili yao na kwamba wanaishi kwa kusikia 
zaidi ya kujitambua.
Katika hali ya kawaida kila mwanadamu ameumbwa kwa njinsi yake na 
inapotokea kushabihiana basi ni bahati, lakini mara nyingi usawa 
hupatikana kwa mmoja kujifunza au kusaidiwa kufikia kiwango cha mtu 
anayemuhitaji kuwa nae katika maisha hasa ya kimapenzi. Jambo hili 
wataalamu wanasema kuwa miili iko tayari kutii mafunzo na kubadilisha 
tabia zake kulingana na utashi wa mhusika.
Tatizo kubwa lililopo kwa wapenzi wengi wanaolalamikia upungufu wa 
nguvu ni kwamba maisha yao wanayachezea kwenye viwanja vya wenzao 
wanaokutana nao katika vijiwe na sehemu za kazi.
Usikivu wa mazungumzo toka kwa wanaume wengine wenye uwezo wa 
kwenda mara nne hadi saba katika tendo au wanatumia dakika arobaini 
kufika kileleni umewafanya wanaume wengi kujihisi tu kuwa wao wanakasoro
 eti kwa kuwa huishia mara mbili au moja katika kufanya tendo.
Dhana ya kujiona ni mwenye kasoro inapojengeka akilini mwa 
mwanaume, huchipua hofu na hatimaye kumfanya ashindwe kabisa kusisimka 
anapofikiria au kukutana na mwanamke. Matokeo ya hangaiko la akili 
hushusha uwezo wa mwili na kumuongoza mtu kwenye kuwaza ugonjwa kisha 
kukimbilia hospitali au kwa waganga kutafuta tiba ya ugongwa ambao 
kimsingi hanao.
Lakini ukweli uko wazi kwamba  kukimbilia kutafuta uwezo wa 
kufanya mapenzi mara sita au saba hakumfanyi mwanaume awe mlinganifu 
mwenye kusifiwa na wanawake wengi, kwani si wanawake wote wana uwezo wa 
kufanya mapezi kwa raundi hizo na si wote wanapenda kutumia takika 30 
kucheza mpira wa kikubwa, wengine hukinai mapema na huona kero kuwa na 
wanaume ving’ang’anizi wenye sifa za kuganda wanapopewa.
