Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye ni 
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Assah Mwambene leo jijini Dar es 
Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa 
Idara hiyo amekanusha taarifa zilizoandikwa kwenye mtandao wa “twitter ”
  na  wanyarwanda kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. 
Jakaya Mrisho Kikwete ni shemeji wa aliyekuwa Rais wa Rwanda Juvenal 
Havyarimana. 
“Taarifa hizi haina ukweli wowote na 
zinalenga kumpaka matope Rais Jakaya Mrisho Kikwete,” amesema Mwambene 
na kufafanua kuwa lengo la mitandao ya kijamii ni kuhabarisha na 
kuelimisha umma wala siyo kupotosha jamii kwa kuandika habari zisizo na 
ukweli wowote.
Madai  hayo  yaliandikwa  jana  na 
 mitandao  ya  Rwanda  wakidai  kuwa  mama  Salma  Kikwete  ni 
 Mnyarwanda  na  ni  binamu  wa  aliyekuwa  rais  wa  zamani  wa 
 Rwanda.
