Alhamisi, 15 Agosti 2013

SHEKHE PONDA HATIMAYE APELEKWA SEGEREA


Hatimaye Sheikh Ponda Issa Ponda leo majira ya saa nn Asubuhi  amepelekwa katika Gereza la Segerea.

Kwa mujibu wa shuhuda wetu aliyekuwepo eneo la tukio ameipasha munirablog kwamba ilipofika majira ya saa nne Asubuhi walikuja Maaskari na kumchukuwa Sheikh Ponda na kumpeleka Gerezani Segerea.

,"Aah wamekuja Maaskari wengi wakatufukuza fukuza wakaingia wodini wakaongea na Daktari wake,wakaandika andika kisha wakamchukuwa na majeraha yake,wala usisumbuke kuja kumuona,hapa hayupo yupo Segerea",alisema mpashaji wa habari hizi.

Sheikh Ponda alifikishwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha mifupa (MOI) siku ya Jumamosi ya tarehe 10/08/2013 Saa saba mchana kwa ajili ya matibabu akitokea mkoani Morogoro baada ya kupigwa Risasi na wanao adaiwa kuwa ni polisi,lakini Jeshi la Polisi kupitia kwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro limekanusha madai hayo.