Hatimaye Sheikh Ponda Issa Ponda leo majira ya saa nn Asubuhi  amepelekwa katika Gereza la Segerea.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu aliyekuwepo 
eneo la tukio ameipasha munirablog kwamba ilipofika majira ya saa nne 
Asubuhi walikuja Maaskari na kumchukuwa Sheikh Ponda na kumpeleka 
Gerezani Segerea.
,"Aah wamekuja Maaskari wengi 
wakatufukuza fukuza wakaingia wodini wakaongea na Daktari 
wake,wakaandika andika kisha wakamchukuwa na majeraha yake,wala 
usisumbuke kuja kumuona,hapa hayupo yupo Segerea",alisema mpashaji wa 
habari hizi.
Sheikh Ponda alifikishwa Hospitali ya 
Taifa ya Muhimbili kitengo cha mifupa (MOI) siku ya Jumamosi ya tarehe 
10/08/2013 Saa saba mchana kwa ajili ya matibabu akitokea mkoani 
Morogoro baada ya kupigwa Risasi na wanao adaiwa kuwa ni polisi,lakini 
Jeshi la Polisi kupitia kwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro 
limekanusha madai hayo.